Wednesday, September 10, 2014

TIGO WAZINDUA TIGO WEKEZA,WATUMIAJI WA TIGO PESA SASA KUPATA FAIDA KATIKA ACCOUNT ZAO

Kampuni  ya mawasiliano ya simu za mkononi ya TIGO Tanzania leo imekuwa kampuni ya kwanza duniani kuzindua huduma inayowapa watumiaji wa tigo pesa fursa ya kupata gawio la faida kwenye account zao kulingana na kiwango cha fedha kilichopo.

   Akitangaza huduma hiyo ya TIGO WEKEZA meneja mkuu wa Tanzania DIEGO GUTIEREZ amesema kuwa zaidi ya wateja million 3.5 wa tigo pesa watanufaika na malipo hayo ambayo yatatolewa mara nne kwa mwaka kila baada ya miezi mitatu.

       Ameongeza kuwa Hii ina maana kuwa tigo pesa haitakuwa tena huduma ya kupokea  na kutuma pesa tu kama ilivyo hivi sasa bali ni njia mojawapo kujipatia kipato cha ziada kupitia huduma ya tigo wekeza.


        Ikumbukwe kuwa wiki iiyopita kampuni hiyo ilitangaza kutoa gawio la shilingi billion 14.25 kwa wateja wake wa tigo pesa kutoka katika mfuko wake wa fedha za account ya tigo pesa kitendo kilichoifanya kuwa kampuni ya kwanza duniani  ya simu kutoa gawio kupitia huduma ya kutuma na kupokea pesa ambapo gawio hilo liliidhinishwa na benk kuu ya Tanzania (BOT).

      Kwa maelezo ya meneja mkuu wa tigo amesema kuwa watumiaji wa tigo pesa watakuwa na nafasi ya kuchagua iwapo watataka kupokea au kuchangia gawio hilo kwa taasisi isiyo ya kiserikali,kutokana na sababu zao binafsi za kiutamaduni au kiimani,ili kupata huduma hiyo mteja atatakiwa kutuma ujumbe mfupi wenye neno WEKEZA kwenda namba 15514 ambapo atapata maelezo zaidi.

        Aidha katika hatua nyingine mkuu wa shirika linalosimamia huduma za mawasiliano ya simu duniani (GSMA) TOM PHILLIPS ameitumia tigo salamu za pongezi akisema kwamba huduma hii mpya ni mfano mwingine wa jinsi ambavyo secta ya mawasilano inachangia katika kuleta maendeleo ya kijamii na kifedha katika jamii.

   

No comments: