Wednesday, October 1, 2014

KAMPUNI YA BERGER PAINTS INTERNALIONAL WALIA NA KODI KUBWA YA SERIKALI

     Kampuni ya rangi ya berger paints international LTD imeshauri serikali kupunguza kodi ya viwanda katika ukuaji wa uchumi na viwanda nchini.

   Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo MEHBOOD BHARWAN amesema kumekuwa na utozaji mkubwa wa kodi ikiwemo kulipa kodi mara tatu zaidi ya zamani hali ambayo amesema inapelekea kufa kwa viwanda nchini.


        Aidha BHARWAN amesema kuwa BERGER PAINTS ni moja inayozalisha bidhaa zenye ubora zaidi ambapo kampuni hiyo inajihusisha na utengenezaji wa rangi ya (robialak)yenye matawi mbalimbali hapa nchini ikiwemo Dodoma na arusha.


        Mkurugenzi huyo ameiomba serikali kuangalia mfumo wa ulipajhi kodi upya kwa kupunguza idadi ya kodi inayotozwa kwa sasa na pia kurejkebisha miundombini hususani barabara ili bidhaa ziweze kufika sehemu husika kwaq muda muafaka kwani secta hiyo ndio mhimili katika ukuaji wa uchumi wa taifa. 

No comments: