Wednesday, October 15, 2014

TIGO YAZINDUA HUDUMA MPYA YA WELCOME PACK

Mkuu wa mkoa wa Iringa Mh. Dkt. Christine Ishengoma akipata maelezo toka kwa mfanyakazi wa kampuni ya Tigo juu ya huduma zitolewazo ndani ya basi la kidijitali la Tigo kwenye uzinduzi wa kifurushi kipya cha Tigo welcome pack mkoani Iringa. Kifurushi inatoa muda wa maongezi wa dakika 20, mb175, sms bila kikomo na shilingi mia 500 kwenye akaunti yake ya tigopesa, yote hayo kwa shilingi 1000 mteja atakaponunua laini yake ya Tigo.


Msanii Lucas Mhavile maarufu Joti akiwapa burudani wakazi wa mkoa wa Iringa kwenye uwanja wa samora hii ni sehemu ya burudani zitolewazo kwenye kampeni ya kifurushi kipya cha Tigo cha welcome pack.


Msanii Slivery Mujuni maarufu Mpoki akiwapa burudani wakazi wa mkoa wa Iringa waliofurika kwenye uwanja wa samora hii ni sehemu ya burudani zitolewazo kwenye kampeni ya kifurushi kipya cha Tigo cha welcome pack.

Timu ya Mkoa wa Iringa iliyoshiki mashindano ya shimiwi ikiingia kwenye basi la Tigo la kidijitali kupata maelezo ya huduma zitolewazo na Tigo ndani ya basi hilo kwenye uwanja wa Samora  mkoani Iringa, hii ni sehemu ya uzinduzi wa kampeni ya kifurushi kipya cha Tigo cha welcome pack.

 Msanii Joseph Haule maarufu Professor J akiwapa burudani wakazi wa mkoa wa Iringa waliofurika kwenye uwanja wa samora hii ni sehemu ya burudani zitolewazo kwenye kampeni ya kifurushi kipya cha Tigo cha welcome pack.

Mkuu wa mkoa wa Iringa Mh.Dkt. Christine Ishengoma akisalimiana na Mkurugenzi mkuu wa Tigo kanda ya kusini Bw. Jackson Kiswaga wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kifurushi kipya cha tigo cha welcome pack mkoani Iringa, kifurushi hicho kitamwezesha mtumiaji wa Tigo kupata muda wa maongezi wa dakiak 20, mb175,sms bila kikomo na pesa shilingi mia 500 kwenye akaunti yake ya tigopesa, yote hayo kwa shilingi 1000 mteja atakaponunua laini yake ya Tigo.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tigo ya zindua huduma mpya ya ‘Welcome Pack’
.Tigo Tanzania leo imezindua kifurushi kipya cha ‘Welcome Pack’ ambayo itawezesha wateja wake kupata huduma ya intanet, SMS, na kupiga simu kwa bei nafuu. Uzinduzi wakifurushi hichi pia inaenda sambamba na kampeni maalum yenye nia ya kuwa elimisha watu na kuwapa fursa ya kushuhudia bidhaa na huduma mbalimbali itakayofanyika katika mikoa 10 nchini. 
Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni hii iliyofanyika katika Uwanja wa Sokoine mkoani Iringa, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mheshimiwa Dk. Christtine Ishengoma aliipongeza sana mchango wa Tigo katika kuleta maendeleo kwa watu wa Iringa na Tanzania kwa ujumla kwa kuwekeza  katika sekta ya mawasiliano ambayo imekuwa  kama kichocheo kikubwa katika kuleta maendeleo ya  kiuchumi na kijamii kwa watu hususan wa mikoani.
“Suala la kwamba kifurushi cha Welcome Pack itawapatia Nwananchi fursa ya kupata dakika 20 za muda wa maongezi, MB 175 zakuperuzi katika intanet, SMS zisizo na kikomo na Tsh 500 katika akaunti yake mpya ya TigoPesa, yote hayo kwa Tsh 1000 kama gharama  ya kununulia laini ya simu itawapatia wateja nafasi nzuri yakuwasilia na zaidi na kwa gharama  nafuu,”alisema Dk. Ishengoma.
“Napenda kuchukua nafasi hii kutoarai kwa wananchi wote wa Iringa kuchangamkia  kifurushi hiki maalum kutoka Tigo kwaajili ya kuendeleza shughuli zao za kiuchumi na kijamii hapa mkoani nap engine. Tumieni muda wa maongezi, intanet, SMS zabure kuwezesha miamala ya kibiashara na kupata elimu ya kibiashara mtandaoni, vitu ambavyo mwisho wa siku vitawasaidia kuongeza uzalishaji na kupata masoko ya kibiashara,” alisema Mkuu huyo wa mkoa.
Dk. Ishengoma pia alisifia kampuni ya Tigo kwa hatua yao ya kuanzisha Basi la Kidijitali la Tigo lenye uwezo wakuwapatia Watanzania elimu kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali zito lewazo na kampuni hiyo kama Tigo Kilimo, Tigo Bima, TigoPesa, Application ya Hesabati kwa wanafunzi wa sekondari, na Facebook ya Bure kwa Kiswahili.
“Ni dhahiri kwamba ujanawazo hili la kibunifu litasaidia kuongeza elimu ya kidijitali kwaWatanzania hasahasa wale wa vijijini, ambayo moja kwamoja inachangia katika ufanikishwaji wadira ya kampuni yenu yakuwezesha maisha yakidijitali nchini,” alisema Dk. Ishengoma.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tigo wa Kanda za Juu Kusini, Joseph Kiswaga alisema kwamba kampuni ya Tigo inayofuraha kutangaza uzinduzi rasmi wa kampeni ya Welcome Pack ambayo itawazawadia wateja wa Tigo watakaojiungana mtandao huo kwa mara ya kwanza kwa kununua laini za Tigo.
Alisema, “Kampeni ya Welcome Pack itakuwepo kwa muda wamie zimi tatu, ambapo misafara zaidi ya 70 ikiwemo basi la Tigo la Kidijitali litatembelea miji 70 na vijiji Zaidi ya 100 ndani ya mikoa 10 tofautii kiwemo Mbeya, Iringa, Dodoma, Arusha, Kilimanjaro, Kagera, Mwanza, Shinyanga, Kigoma na Mtwara.”
“Misafara hii yataambatana na tamasha la muziki katika kila siku ya mwisho wamsafara utakao fanyika kila Jumapili. Wasanii wa Bongo Fleva watakaotoa burudani ni pamoja na Profesa J, Joh Makini, Shah, Mheshimiwa Temba na Chege, Madee na Izzo Business. Tunapenda kuchukua fursa hii kuwa karibisheni nyote,” alimalizia kwa kusema Kiswaga.
Mwisho.    

No comments: