Thursday, November 27, 2014

ESCROW BUNGENI--HUU NDIO UTETEZI WA WAZIRI MUHONGO.


Ameanza kwa kuomba radhi kama jana kulikuwa na usumbufu wa umeme na anawaagiza mameneja wote wa TANESCO wasikate umeme.

Anatoa pongezi juu ya mjadala wa Escrow, mengi yamesemwa na niwakati wa kuanza mjadala kujua ukweli, Shukraan kwa CAG, TAKUKURU kwa uchunguzi. Pia nawashukuru PAC, jana tulitulia kuwasikiliza PAC na leo tutulie tusikilize utetezi wangu

Miaka ya 90 tulikuwa tuna upungufu wa umeme kutokana na maji, 1994 serikali ilitoa kazi ya uwekezaji kwa IPTL ilikuwa inamiliwa na VIP ya Tanzania iliyokuwa na 30% na Mechmar ya Malaysia 70%.

Kulingana na mkataba, majukumu ya IPTL yalikuwa kujenga, kumiliki na kuendesha hivyo utaifashaji utaiingiza serikali katika matatizo makubwa ikiwemo kushtakiwa kimataifa pia itafukuza wawekezaji binafsi. TANESCO na IPTL walisainiana mkataba wa miaka 20, hata hivyo uzalishaji haukuanza mara moja kutokana na mgogoro ulioibuka baina ya TANESCO na IPTL

Ilianza kuzalisha umeme 2002 hivyo mkataba ukaanza kuhasabiwa hapo, kutokana na mgogoro ikafunguliwa Escrow Account na escrow ilizungumziwa toka mkataba wa 1995.

2004 TANESCO ilifungua shauri kupinga tozo la capacity charge
Taarifa hio sio kweli kwani TANESCO haijawahi kufungua kesi yoyote dhidi ya standard charted kamailivyosemwa na PAC. Kesi hiyo ilifunguliwa na Standard charted na ilikuwa haihusu capacity charge. Hamna kokote mkataba kati ya standard charted na TANESCO.

Makinda ameingilia na kusema ripoti itatolewa baada ya wabunge kudai ripoti.

Muhongo anaendelea
Uwiano wa mtaji ni 70 kwa 30, na uamuzi haujabadilishwa na mahakama yoyote. 2004 kampuni ya Mkono and CO advocates iliishauri TANESCO iendelee kupinga capacity charge London. Hata hivyo, tanesco haikuishauri TANESCO kufungua kesi za TANZANIA wala mahakama ya kimataifa. Hadi 2013 jaji Utamwa anatoa hukumu ya mgogoro wa wanahisa wa IPTL kulikuwa hamna kesi yoyote kuhusu tozo ya IPTL. 

UUZAJI WA HISA ZA VIP
Kutokana na kutokubalina Mechmar iliishauri VIP ifungue shauri. VIP ilifungua shauri Tanzania ikiomba IPTL ifilisiwe. Uamuzi ulitolewa kwa shauri la VIP. Chini ya Kimario, alpewa mfilisi wa mda kulinda mali za IPTL, kufanya uchunguzi ili mahakama iweze kutoa uamuzi. Uamuzi ulitoka IPTL iweke kwenye ufilisi kamili chini ya RITA. Hukumu ilipingwa mahakama ya rufaa ikianisha dosari katika uamuzi wa mahakama kuu na Standard charted Hong Kong. Mahakama ya rufaa ilikubaliana na hoja hiyo na ilipelekwa tena kwa mfilisi wa muda kukusanya madeni, kusuluhisha mogogoro na kuendesha mitambo ya IPTL kwa niaba ya IPTL. 

Serikali haiwajibiki kuingilia hisa za makampuni binafsi, mauzo ya hisa yaliyofanyika nje ya nchi yatatambuliwa tu endapo yatatambuliwa na BRELA. Uhamishaji wa hisa 7 ulisajiliwa hapa nchi. Kamati katika uthibitisho huo inakubali hisa za Mechmarr unamilikiwa na PAP

Hiza saba za IPTL unatambuliwa pia na Standard Charted, Kama PAP haimiliki asilimia sabini kwanini wana makubaliano na standard charted ya Uingereza.

Ilifilisiwa Malasia na sio Tanzania, madai ya standard charted dhidi ya TANESCO ni kwa sababu IPTL waliweka dhamana mtambo wa kuzalishia umeme, Lakini benki ya Hong Kong ilikosa sifa ya kufungua shauri Tanzania hivyo ilifungulia Uingereza

VIP chini ya usuluhishi wa RITA iliuza hisa zake PAP kwa dola milioni 70 na ndivyo ilivyomaliza mgogoro wa IPTL. Mimi sio dalali wa hii biashara bali ni dalali wa(anasema mambo mazuri aliyoyafanya)
Makinda amekuwa mkali kidogo kwa Muhongo asome taarifa na asiseme ambayo hayamo.

ESCROW ACCOUNT
TANESCO kwa ushauri wa mkono walitoa hoja kuwa gharama za kununua umeme na makadirio ya mtaji walitoa notisi(invoice disputes notice) ya kupinga usahihi wa malipo. Alietoa ushauri ni kampuni ya Mkono, 2006 serikali ulisaini mkataba wa kufungua account ya Escrow.

MMILIKI WA FEDHA YA ESCROW
Account ya Escrow ilipaswa kuwa na bilioni 306 zilizowekwa na TANESCO. PAC walitoa mapendekezo kuwa imethibitisha kuwa mchakato wa kutoa pesa Escrow umegubikwa na mchezo mchafu na kutakatishwa na benki mbili nchi

TAHADHARI ZILIZOCHUKULIWA
Serikali ilichukua kinga kutoka IPTL, kwa mujibu wa kinga IPTL itawajibika yakitokea madai yoyote na ilipitiwa na mwanasheria mkuu wa serikali. (Yoyote anaedai chochote aende IPTL)

PAC wameeleza serikali haikuchukua tahadhari ya kutosha juu ya madai mapya kama yangejitokeza kitu ambacho sio kweli.

DHANA YA MADAI YA BILIONI 321
Madai kwamba IPTL inaidai IPTL 321 Bilioni, bodi ya TANESCO imekana kuyatambua madai haya na vitabu vya TANESCO vinavyokaguliwa na CAG hakionyeshi madai haya.

Madai yaliyowasilishwa na mufilisi, yalitakiwa kuhakikiwa lakini hayakuhakikiwa na hayakuwa na uhalali wowote.

Kamati ya PAC, wamesema yana uhalali japo uhalali wake unategemea maamuzi.

No comments: