Tuesday, November 11, 2014

HABARI MPYA KUTOKA CUF

Na Karoli Vinsent

           JUMUIYA ya Vijana na Wanawake wa Chama cha Wananchi CUF kimetangaza uchaguzi wa ngazi za matawi,kata,wilaya kwa ujumla  ambapo mpaka mwishoni mwa  Novemba mwaka huu chama hicho kitakuwa kimekamilisha uchaguzi  kwa wilaya zaidi 80 kwa Zanzibar na Tanzania bara,
     
  Na uchaguzi wenyewe utafanyika kuanzia tarehe 15 mwezi 11 mwaka huu hadi tarehe 22 mwezi 11 mwaka huu ambapo Jumuiya ya Vijana kutoka chama hicho pamoja na Jumuiya ya Wanawake zitakuwa zimekamilisha chaguzi zake za ngazi ya Wilaya.



              
         Akitangaza Uchaguzi huo leo Jijini Dar Es Salaam wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari,Naibu Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Vijana wa Chama cha Wananchi CUF(JUVICUF),Hamidu Bobali amesema uchaguzi huo utakuwa huru na ukizingatia suala zima la Demokrasia na kutoka fursa kwa vijana na wanawake kuomba nafasi mbalimbali za uongozi kwa ajili ya kuwakilisha Jumuiya zao katika  ngazi za juu za maamuzi katika chama hicho.
         
          Akaongeza kuwa uchaguzi huo utazingatia katiba na kanuni ya chama hasa kwa upande wa vijana ambapo umri wa mgombea ni hutakiwa kuzidi miaka 35, na jumuiya ya wanawake  sifa kubwa ni kuwa mwanamke mwanachama umri ni kuanzia miaka 18 na kuendelea.
        
           Vilevile Bobali alizidi kusema form za kuomba nafasi ya Mwenyekiti,makamu na mabaraza ya Vijana pamoja na wanawake Taifa yataanza kutolewa   kuanzia tarehe 15 mwezi 11 mwaka huu hadi tarehe 22 mwezi 11 mwaka huu,katika wilaya zote,na akawata vijana wote kujitokeze ili kugombania nafasi hii yenye uwezo wa kukijenga chama hicho.
         
         

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya wanawake wa Chama hicho Nuru Awadhi Bafadhil aliwataka wanawake kujitokeza kwa wingi katika chaguzi hizi ili kuweze kukijenga chama hicho kikongwe cha upinzani nchi.

No comments: