Na Karoli
Vinsent
SERIKALI
nchini imsema haiwezi kuingilia mgogoro unaoendelea kwenye Bunge la Afrika
mashariki kati ya Mbunge wa Bunge hilo kutoka Tanzania Shyrose Banji na Wabunge
wenzake kutoka nchi zengine zinazounda umoja huo wa Afrika mashariki na kusema
kanuni za Bunge hilo, zinakaza serikali ya nchi yeyote kuingilia kazi au mambo
ya bunge hilo.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es
Salaam na Mkurugenzi wa Siasa na Usalama wa kutoka Wizara ya Ushirikiano na
Uhusiano Afrika Mashariki, Steven Mbundi wakati wa mkutano na waandishi ambapo
Mbundi alisema kwa sasa serikali ni kama
imepigwa kufuli kuhusu sakata hilo kutokana na kanuni wazilijiwekea kwenye
Bunge hilo.
“Kwanza niseme hili sakata la mbunge wetu
limekuwa likiandikwa sana kwenye kwenye magazeti na ukweli huku hivi sisi
serikali hatuwezi kuingilia suala kwani kanuni za bunge hilo na utaratibi wake
wa kuamua mamo na sisi serikali tutachukua hatua zaidi baada ya Spika wa Bunge
la Afrika Mashariki atakapotua uamuzi”alisema Mbundi.
Mbundi aliongeza kuwa Taarifa
zinazoripotiwa kwenye mitandao ya kujamii na magazeti kuhusu Shyrose Banji kufanya
Fujo kwenye Ndege walipokuwa wanakwenda kwenye Ziara ni za upande Mmoja ambazo
hazijampa nafasi hata mwenyewe kujitetea na kusema ukweli wa Mambo utagundulika
mara tu baada ya kamati iliyoundwa kuchunguza sakata hilo kutoa majibu kwenye
Kikao kichacho cha Bunge hilo.
Na akatabainisha kuwa Serikali nchini ndipo
itakapochukua hatua kwenye Jambo hilo.
Kwa upande
wa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ya Afrika Mashariki be Jocye Mapunjo alisema kwa
sasa Muungano huo wa Afrika Mashariki unatakuwa na tija na wenye kubadilisha
nchi zinazounda Umoja huo kuwa kwenye malengo ya maendeleo.
“Kiukweli nawaomba watanzania wote watambue mchango
wa ushirikiano huu,kwani duniani kote hata kwenye mataifa yaliyoendelea
yamepiga hatua kutoka na mashirikiano kama haya,na ushiriano huu utakuwa na
nafasi ya kuwabadilisha watanzia kuwa katika mipango mizuri ya maendeleo”alisema
Be Mapunjo.
Vilevile Be Mapunjo alisema kwa sasa
wanakaribia kwenye mkutano mkuu wa jumuiya hiyo ambao utafanyika tarehe 30
Novemba mwaka huu huku Nairobi nchini kenya na kusema makutano huo utakuwa na
mambo mengi yenye maendeleo.
Jumuiya ya
Afrika mashariki ni Muunganiko wa Nchi za Tanzania,Kenye,Uganda,Burundi na
Rwanda ambapo Muunganiko licha ya kuwa na changamoto mbalimbali umeleta tija
kwa wananchi wa Jumuiya hizi
No comments:
Post a Comment