Friday, November 14, 2014

TANGAZO TOKA TFF LEO


KUBUNI JEZI MPYA YA TIMU ZA TAIFA MWISHO KESHO
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limekaribisha wabunifu, kubuni mwonekano wa jezi mpya za timu ya Taifa kwa mechi za nyumbani na ugenini ambapo mwisho wa kufanya hivyo ni kesho (Novemba 15 mwaka huu). Ubunifu ni lazima uzingatie rangi za bendera ya Taifa.


Mshindi wa jezi ya nyumbani atapata sh. 1,000,000 (milioni moja), na mshindi wa jezi ya ugenini atapata pia sh. 1,000,000 (milioni moja).

Ubunifu utumwe kwenye anwani ya barua pepe:info@tff.or.tz au uwasilishwe kwa CD au flash zikiwa katika mfumo wa PDF katika ofisi za TFF zilizopo ghorofa ya tatu katika Jengo la PPF Tower, Mtaa wa Ohio na Garden Avenue.

Kwa maelezo zaidi unaweza kuwasiliana nasi kwa simu namba; 0713 210242 au 0714 634838.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

No comments: