Monday, November 10, 2014

ZIARA YA TIGO WELCOME PACK YATIKISA MKOANI KAGERA

1s
Mfanyakazi wa uwanja wa Ndege wa Bukoba Bi Leiner Rogatus akifurahi mara baada ya kununua simu Huawei 330 kwa sh 130,000 Nje ya uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba ambao kampuni ya simu za Mkononi ya Tigo ilikuwa ikitambulisha huduma zake mbalimbali kwenye kampeni ya Tigo welcome pack mwishoni mwa wiki
2sMeneja bidhaa wa Tigo Bw.Robert Paul akiongea na wafanyabiashara wa soko la Kaisho wilayani Karagwe kuhusu Tigo Kilimo hii ni moja ya kampeni za Tigo welcome pack zinazoendelea mikoa mbalimbali nchini.
4sMsanii wa bongo fleva Sunday Mjeda maarufu Linex akitoa burudani kwenye tamasha la Tigo welcome pack lililofanyika kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, kampeni ya welcome pack inawawezesha wateja wa Tigo kujua huduma mbalimbali zitolewazo na kampuni ya Tigo.

5sWasanii wa kundi la Original Komedi wakitoa burudani kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba wakati wa kampeni ya kifurushi cha Tigo welcome pack, Kifurushi hicho kitamwezesha mtumiaji wa Tigo kupata muda wa maongezi wa dakika 20, mb175,sms bila kikomo na pesa shilingi mia 500 kwenye akaunti yake ya tigopesa, yote hayo kwa shilingi 1000 mteja atakaponunua laini yake ya Tigo
6sWasanii Emmanuel Mgaya Maarufu Masanja Mkandamizaji na Slivery Mujuni maarufu Mpoki wakitoa burudani kwa wakazi wa Bukoba waliofurika kwenye uwanja wa Kaitaba wakati wa onesho la Tigo welcome pack
8sMsanii wa bongo fleva Hamisi Mwinyijuma a.k.a MwanaFA akiwapa shoo wakazi wa mji wa Bukoba waliofurika kwenye uwanja wa Kaitaba wakati wa tamasha la Tigo welcome pack.
9sSehemu ya umati uliyohudhuria tamasha kubwa la Tigo welcome pack mjini Bukoba.
10sMeneja bidhaa wa Tigo Bw.Robert Paul akiongea na waandishi wa habari kwenye uwanja Kaitaba.

No comments: