Meneja mkuu wa tigo Tanzania CECILE TIANO akizngumza na wanahabari mapema leo jijini Dar es salaam |
Kampuni ya mawasiliano ya tigo nchini Tanzania imepanga
kutumia million 120 za kimarekani sawa na 221bn mwaka huu katika kupanua
mtandao wake na kuimarisha kiwango cha ubora wa huduma zake.
Akieleza mipango ya kampuni hiyo kwa mwaka 2015
kaimu meneja mkuu wa tigo Tanzania CECILE TIANO amesema kuwa kiasi hiki cha
uwekezaji ni ongezeko la asilimia 20 kutoka dola za kimarekani 100 sawa na
184bn ambazo kampuni hiyo iliwekeza mwaka jana katika upanuzi na uimarishaji wa
mtandao wake wa mawasiliano.
Amesema kuwa ongezeko la uwekezaji linaonyesha
juhudi za kampuni hiyo kwa wateja wake na kiwango cha huduma zao ambacho ni
zaidi ya matarajio yao na pia inawapa watanzania fursa ya upatikanaji wa huduma
za mawasiliano ya simu ndani ya nchi.
Kulingana na maelezo yake anasema kuwa mwaka 2014 ni
msimu uliokuwa wa mafanikio ambapo tigo ilijivunia record ya asilimia 30 kwa
ongezeko kwa wateja wake waliojiunga mwaka jana ilipelekea idadi ya wateja
kuongezeka kutoka million saba hadi million tisa.
Aidha amesema kuwa kampuni ya tigo Tanzania inataka
iendelee kutanua wigo wa mtandao huo kwa kuweka minara 787 mipya nchini nzima
na baadhi ya minara hiyo itakuwa na 3g na 4g . ambapo amesema kuwa minara hiyo
itapelekea kuongezeka kwa upatikanaji wa uduma za tigo vijijini na pia itaongeza
upatikanaji internent wa wateja wa mtamndao huo.ambapo amesema kuwa tigo kwa
sasa ina minara 2,000 nchi nzima
Bi TIANO amesema kuwa mipango mingine ya kampuni
hiyo kwa mwaka huu ni kuhusu kuongeza mara mbili idaadi ya maduka ya huduma kwa
wateja kutoka maduka 42 mpaka maduka 100 katika kuhakikisha kuwa huduma hizo
zinawafikia wateja wengi nchini.
Aidha akijibu swali la mwandishi wa mtandao huu
kuhusu kupungua ghafla kwa vifurushi vya mtandao wa internent bila taarifa
mkurugenzi huyo ameesema kuwa Tanzania bado ni nchi ambayo ina gharama za chini
sana katika matumizi ya internent ukilinganisha na nchi nyingine za Africa ambapo
amesema pia chanzo kingine cha kupunguza huduma hiyo ni kutokana na tozo kubwa
ya kodi wanatotozwa na serikali kwa sasa ambapo amesema hata hivyo sio muda
muafaka wa kulizungumzia swala hilo kwani tayari wamepata malalamiko kutoka
TCRA kuhusu kukatisha huduma hizo bila taarifa na wapo katika mazungumzo na
waatanzania watajuzwa kinachoekndelea
No comments:
Post a Comment