Saturday, April 11, 2015

KUNA KITU ULISKIA LEO KUHUSU HAWA WATU?--NI UONGO-UKWELI HUU HAPA


Huwenda leo umeskia habari mbalimbali kwenye mitandao humu zikisema kuwa kiongozi mkuu wa chama cha ACT wazalendo mh ZITTO KABWE amempeleka mwenyekiti wa chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA  mh FREMAN MBOWE mahakamani kisa ni kutumiana ujumbe mfupi wa simu wa vitisho.


Habari hizo zilikuwa zinasema kuwa mwenyekiti wa CHADEMA alimtumia ujumbe mfupi wa maandishi mh ZITTO KABWE ujumbe ambao ulikuwa unamtuhumu kuwa anatumika na chama cha mapinduzi na serikali NA PIA ANAITUMIA act KAMA DARAJA TU ILA ANAENDA KUJIUNGA ccm na maneno ya kumtisha mengi jambo ambali likamfanya MH ZITTO kwenda kutoa ripot mahakamani kwa usalama wake ila habari hizo hazikutaja ni mahakama gani kesi hiyo imepelekwa.


   Sasa ukweli uko hivi mtandao huu uliposoma habari hizo kwenye baadhi ya blog ukaamua kumtafuta afisa habari wa chama cha ACT ambaye ametuambia kuwa hakuna ukweli wowote wa habari hizo ambapo amesema hata wao wanashangaa story hiyo inayoenea ina lengo gani zaidi ya kuwagombanisha watu hao wawili.

Ndugu mwandishi hakuna ukweli wowote kaka wa habari hizo hata sisi tunazisikia tu kwa juu juu hatujui chanzo cha habari hizo,ila tunafwatilia kujua mtunzi wa habari hizo,ZITTO kama mnavyojua yupo kwenye ziara ya kuimarisha chama chake mikoani na wala hajafika mahakama yoyote  sasa tunashangaa kwa mambo hayo kuzushwa kiajabu ajabu.
Mitandao mingi ilidai kuwa haya ni maelezo ya zitto ila hakuna ukweli wowote

"NIMEPOKEA UJUMBE WA SMS KATIKA SIMU YANGU UJUMBE AMBAO SIO MZURI KIUKWELI NA UJUMBE UNAONESHA KUA UMETOKA KWA MWENYEKITI WA CHADEMA FREEMAN MBOWE NAAMINI UJUMBE UMETOKA KWAKE KWAKUA NAMBA YAKE YA SIMU NINAYO NA NILI SAVE KATIKA SIMU YANGU YA MAWASILIANO KWA JINA LA MKT. MBOWE KWA MAANA YA MWENYEKITI MBOWE HIVYO NILIVYOPATA UJUMBE JINA LILITOKEA HILO LA MTUMAJI NA KUJUA UJUMBE UMETOKA KWAKE NA NILIPO ANGALIA CENTER NUMBER IMETUMIKA YA VODACOM NIKAJARIBU KUMPIGIA HAKUA AKIPOKEA SIMU ZANGU LENGO LA KUMPIGIA NI KUTAKA KUPATA USHAHIDI NA UHAKIKA ZAIDI WA SAUTI YAKE LAKINI HAKUA AKIPOKEA SIMU ZANGU NDIPO LEO ASUBUHI NIKAWASILISHA HII KESI KATIKA VYOMBO VYA SHERIA ILI KUWEKA USALAMA JUU YA JAMBO HILI NIMEUMIA SANA KUAMBIWA MIMI NI KIBARAKA WA CCM PIA NIMEAMBIWA KUA NIMEJIUNGA ACT WAZALENDO KAMA DARAJA TU KUWAHADAA WANANCHI ILI NIHAMIE CCM

No comments: