Saturday, April 25, 2015

TIZAMA TUKIO NZIMA LA TUZO ZA WANAHABARI JANA MLIMAN CITY

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa hafla ya Utoaji Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari, iliyofanyika jana usiku April 24, 2015 kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi mfano wa Hundi ya Sh. Milion tatu na Laki Nane (M.3.8) mshindi wa jumla katika kinyang’anyiro cha Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT), Mwandishi wa habari wa Gazeti la Mwananchi, Mkinga Mkinga, wakati wa hafla hiyo ya utoaji tuzo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, jana usiku Aprili 24, 2015. Kushoto ni Rais wa Baraza la Habari Tanzania, Jaji Mstaafu Robert Mihayo na Generali Ulimwengu. Picha na OMR


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo  mshindi wa pili wa jumla katika kinyang’anyiro cha Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT), Mwandishi wa habari wa Gazeti la The Citizen, Lucas Liganga, wakati wa hafla hiyo ya utoaji tuzo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, jana usiku Aprili 24, 2015. Picha na OMR



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi mfano wa Hundi ya Sh. Milioni kumi (M. 10) Mwandishi wa habari wa siku nyingi mkongwe, Generali Ulimwengu, wakati wa hafla hiyo ya utoaji tuzo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, jana usiku Aprili 24, 2015. Kushoto ni Rais wa Baraza la Habari Tanzania, Jaji Mstaafu Robert Mihayo na (kulia) ni Mke wa Generali Ulimwengu. Picha na OMR


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na wanahabari waliopata Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa habari, zilizotolewa jana usiku Aprili 24, 2015 wakati wa hafla hiyo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na wanakamati wa maandalizi wa hafla hiyo baada ya kumalizika hafla hiyo kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam jana usiku Aprili 24, 2015. Picha na OMR.
PICHA NYINGINE ZA TUKIO HILO ZIPO CHINI







No comments: