Sunday, May 31, 2015

DIWANI WA CCM AWASHUKURU MABALOZI KATIKA KATA YAKE KWA KAZI KUBWA WANAYOFANYA

Diwani wa kata ya Ndugubi iliyopo katika Jimbo la Kinondoni Mh CHARLES MGONJA akizungumza na mabalozi wa mitaa mbalimbali waliojitokeza katika kikao hicho ch pamoja cha kujadili maswala mbalimbali ya maendeleo yanayofanyika katika kata yao.kikao ambacho kilifanyika katika shule ya secondary Turiani

 Diwani wa kata ya Ndugubi iliyopo katika Jimbo la Kinondoni mh CHARLES MGONJA leo amekutana na mabalozi wote waliopo katika kata yake kwa lengo la kuwakutanisha kwa pamoja kujadili  kuhusu kazi ambazo zinafanywa na diwani huyo pamoja na kuwashukuru madiwani hao kwa kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa mambo ya maendeleo katika kata hiyo.
Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu nje ya mkutano huo amesema kuwa kumekuwa na malalamiko kutoka kwa mbalozi hao kuwa wamekuwa hawapati nafasi kama hiyo ya kukutana na kujadili kwa pamoja na viongozi walio juu yao pamoja na kazi kubwa wanayoifanya,jambo ambalo limemsukuma kuwakutanisha mabalozi hao kujadili kwa pamoja na kuelewa kila kitu ambacho serikali yao inakifanya katika kuwaletea wananchi maendeleo.
Mabalozi mbalimbali waliojitokeza katika kikao hicho
Amesema kuwa ufanisi wa kiongozi wa ngazi za juu za serikali hauwezi kuwa na maana kama hauna mahuziano mazuri na viongozi wa ngazi za chini za wakiwemo mabalozi hao kwani ndio wanaohakikisha kuwa katika mitaa yote kunakuwa na ulinzi wa kutosha na kuimarisha amani katika maeneo yote ya kata hizo.

Akizungumza na mabalozi hao diwani MGONJA ameanisha mambo mbalimbali ambayo serikali yake imefanya katika kata hiyo kama ujenzi wa maabara katika shule za secondary ikiwa ni utekelezaji wa agizo la rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania DK KIKWETE, huku changamoto ikibaki kuwa upatikanaji wa vifaa katika maabara hizo,ujenzi wa barabara katika mitaa mbalimbali ya kata hiyo pamoja na maendeleo makubwa katika secta ya afya na maji.
Akizungumzia joto la uchaguzi ambalo limeanza kupanda kwa kasi ndani ya chama cha mapinduzi amesema kuwa ni nafasi sasa ya wanachama wa chama cha mapinduzi katika kata hiyo kutumia nafasi yao ya kidemocrasia ya kutangaza nia na baadae kugombea katika nafasi mbali mbali za uongozi katika kata hiyo na jimbo kwa ujumla lengo likiwa ni kukisaidia chama hicho kupata viti vingi zaidi vya udiwani na ubunge katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika hapo baadae mwaka huu.






No comments: