Wednesday, May 27, 2015

LHRC WAZINDUA RASMI REPORT YA HAKI ZA BINADAMU YA MWAKA 2014,WAJIVUNIA MIAKA 20 YA MAFANIKIO MAKUBWA

Mgeni rasmi ambaye ni aliyewahi kuwa mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu Jaji Mstaafu Amir Manento akiwa katika picha ya pamoja na mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu nchini LHRC Bi HELLEN KIJO BISIMBA pamoja na wadau mbalimbali waliohudhutia katika hafla hiyo ya yzinduzi wa report ya haki za binadamu kwa mwaka 2014 uzinduzi ulioenda sambamba na miaka 20 ya kituo hicho katika  uangalizi na utetezi wa haki za binadamu

NA EXAUD MTEI
 Kituo cha sheria na haki za binadamu(LHRC) kimezindua report yake ya haki za binadamu ya mwaka 2014 uzinduzi ulioenda sambamba na maadhimisho ya  miaka 20 ya uangalizi na utetezi wa haki za binadamu wa kituo hicho huku wakijivunia miaka 20 yenye mafanikio makubwa katika kueneza haki za binadamu Tanzania.
Akizindua taarifa ya haki za binadamu ya mwaka 2014 hii leo Jijini Dar es salaam  Jaji mstaafu  na aliyewahi kuwa mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu Jaji Amir Manento amesema lengo kuu la kuzindua Taarifa hii ni kujenga uelewa juu ya maswala ya kisheria na Haki za Binadamu na kutoa ushawishi wa kuboresha katiba,kutetea na kuheshimu haki za binadamu nchini.
Amesema kuwa ni mafanikio makubwa ya kujivunia kwa kituo cha sheria na haki za binadamu kufikisha miaka 20 ya utumishi ambao wameonekana wazi kuwa wamewasaidia watanzania wengi katika maswala ya kisheria na haki za binadamu jambo ambalo amesema kuwa ni lazima wapongezwe kwani kazi waliyofanya ni kubwa.

Amengeza kuwa kituo hichi kimekuwa mstari wa mbele katika kufungua kesi mbalimbali ambazo zina maslahi kwa umma ili kushinikiza uwajibikaji,mabadiliko ya sera na pia ulinzi wa haki za binadamu ambapo amesema kuwa ni udhubutu aina yake kufanya hivyo.
Ametaja mashauri ambayo yamewahi kufunguliwa na kituo hicho na kuwasaidia watanzania ni pamoja na shauri dhidi nya waziri mkuu Mh MIZENGO PINDA,shauri la takrima,shauri la kupinga uanzishwaji wa mfuko wa jimbo,shauri la kutaka ulinzi wa kutaka ulinzi wa watu wenye ulemavu wa ngozi na mashauri mengine mengi ambayo yalikuwa na maslahi kwa umma.

Mgeni rasmi ambaye ni aliyewahi kuwa mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu Jaji Mstaafu Amir Manento pamoja na mkurugenzi mtendaji wa kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini LHRC Bi HELLEN KIJO BISIMBA wakizindua rasmi Report ya Haki za Binadamu ya mwaka 2014 Jijini Dar es salaam
Kwa upande  wake Mkurungenzi wa kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Dr Hellen kijo Bisimba amesema kituo cha sheria na haki za Binadamu kimetoa ushauri kwa serikali na wadau mbalimbali kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa katika  Taarifa iliyozinduliwa leo ilikuboresha hali ya haki za binadamu nchini  na kuongeza kuwa  ukiukwaji wa sheria na haki Za binadamu  unatokea kwa sababu ya ukosefu wa elimu.
Amesema kuwa katika Report hiyo imeonyesha maswala kadhaa ambayo bado yamekuwa matatizo makubwa Tanzania yakiwemo maswala ya uwajibikaji wa viongozi pindi wanapokumbwa na kashfa za ufisadi,swala la kuvamiwa na kupigwa kwa askari nchini Tanzania,pamoja na maswala ya haki za makundi mbalimbali wakiwemo watoto na wakina mama.
Aidha katika taarifa hiyo iliyozinduliwa  leo imeangalia maeneo mbalimbali toka mwaka 2002 hadi kufikia mwaka 2014  .kituo cha sheria na haki za binadamu kimetoa mapendekezo mbalimbali kwa serikali ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya haki za binadamu  katika ngazi zote za elimu na  na serikali,  serikali  ichukue hatua za haraka kwa wavunjaji wa sheria na haki za binadamu ili iwe fundisho kwa jamii inayotuzunguka.

No comments: