Friday, May 15, 2015

RED CROSS KILIMANJARO YATOA MISAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO HAI

Wa kwanza kushoto August Temu Mwenyekiti wa Red Cross Kilimanjaro,katikati ni Katibu Tawala Wilaya ya Hai  Zuhura Chikira na Mkurugenzi Wilaya ya Hai Said Ahmed Said Mderu wakipokea msaada  kwa waathirika wa mafuriko.
HAI
MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Said Ahmed Said Mderu amewataka wahanga wa mafuriko  wa kata ya Rundugai na Weruweru  wanaopokea misaada mbalimbali kuitunza na kuitumia ili kuwasaidia katika kipindi hiki kigumu.

Ameyasema hayo leo alipokuwa anapokea misaada  mbalimbali kutoka shirika la Msalaba Mwekundu Kilimanjaro katika kijiji cha Kawaya Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro.

Mderu amesema kuwa  ikiwa wahanga hao wa mafuriko watakuwa wanatumia misaada wanayo pelekewa pasipo utaratibu maalumu utasababisha mashirika mengine pamoja na wadau mbalimbali kusitisha kupeleka hudumu muhimu maeneo hayo ,hivyo ni vema waka onesha hali ya ustaarabu katika kutumia misaada
hiyo.

"itashangaza sana kwa vyandarua vinavyo tolewa kutumika katika  kuvulia samaki au kufugia kuku kama watu wengine wanavyo fanya niwaombeni msifanye hivyo."Alisema Mderu.

Pia amepongeza wadau mbaimbali ambao ni benki ya NMB pamoja na Mbunge wa Hai Freeman Mbowe kwa misaada waliyo toa katika kaya zilizo kumbwa na mafuriko jambo ambalo limewapa matumaini makubwa wananchi hao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shirika la Msalaba Mwekundu Kilimanjaro  August Temu ameserma kuwa watazidi kutoa huduma na misaada mbalimbali kwa wananchi wanao kutwa na majanga mbalimbali ili kuweza kuonesha upendo baina ya shirika na wananchi kwani ni jukumu la shirika hilo kutoa misaada kama hiyo.

Amesema kuwa  mbali na wananchi kutegemea mashirika na wadau mbalimbali bado kuna nafasi kubwa ya wananchi wenyewe kupendana na kusaidiana katika majanga ili kuweza kuonesha uzalendo huku akiwataka wananchi kutoa misaada kama vile mavazi,vyakula na malazi kwa waathirika wa mafuriko hayo.

"Tusipende kila kitu tusaidiwe kutoka nje ya nchi sisi wenyewe tunaweza tukasaidiana kutatua matatizo yetu pasipo kutegemea nje ya nchi hivyo naombeni tuwe na utamaduni wa kusaidiana sisi kwa sisi".Alisema Temu.

Shirika hilo la Msalaba mwekundu limetoa misaada kwa wanakaya wote wa kata ya rundugai na weruweru walio kumbwa na mafuriko hayo ikiwa ni pamoja na mablanketi 125,vyandarua 100,mabeseni 120,ndoo 200 na dawa za kusafisha maji katoni 20.

Tazama picha za upokeaji wa msaada huo kwa waathirika wa mafuriko.



Red Cross wakishusha misaada  kutoka kwenye gari



Baadhi ya misaada ikiwa mbele ya wananchi.


Diwani wa kata ya Machame Wereweru  Idris Mandray akizungumza na waathirika wa mafuriko hayo





Mwenyekiti wa  Red Cross Kilimanjaro  August Temu akizungumza na wananchi hao wakati wa kugawa msaada huo.






No comments: