Friday, May 29, 2015

WAISLAM--HATUHUSIKI HATA KIDOGO NA UGAIDI UNAOENDELEA AFRICA,SOMA HII

Kiongozi Mkuu wa kiroho wa Waislam Dhehebu la SHIA ITHNASHERIYA Tanzania Sheikh HEMED JALALA akizungumza na wajumbe mbalimbali kutoka dini zote waliohudhuria katika kikao hicho Jijini Dar es salaa kikao kilichikua na lengo la kujadili kwa pamoja hatma ya bara la africa na ugaidi unaoendelea humo
Imeelezwa kuwa vitendo vya ugaidi na mauaji yanayofanywa na watu mbalimbali barani  Africa na duniani kwa ujumla hayahusiani hata kidogo na dini ya kiislam kama ilivyokua ikielezwa na wadau mbalimbali kuwa mauaji hayo yanahusiana na imani ya dini ya kiislam.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dare es salaam na kiongozi Mkuu wa kiroho wa Waislam Dhehebu la SHIA ITHNASHERIYA Tanzania Sheikh HEMED JALALA wakati akizungumza katika kikao cha pamoja cha viongozi wa dini zote kikao kilichoandaliwa na chuo cha kidini cha IMAM JAFAR SWADIQ,kigogo Jijini Dar es salaam.
Muwakilishi wa wakiristo katika mkutano huo pastor PRINCE ERASTO IKONGO kutoka pentecoste akizngumza katika kikao hicho ambapo amewataka waumini wa dini za kikristo kuondoa hofu juu ya waislam padala yake wadumishe umoja na amani iiyopo nchini
Amesema kuwa ugaidi katika bara la Africa umekuwa ukitafsiriwa kuwa ni jambo ambalo limekuwa katika msukumo wa dini ya kiislam jambo ambalo amesema kuwa watanzania wanapaswa kuelewa sio sahihi kuwatuhumu waislam kwa ugaidi kwani hakuna kitabu chochote kinachoruhusu muislam kufanya mauaji kwa mwadamu mwenzake.
Amefafanua kuwa mivutano na Ugaidi uliyopo barani Africa umekuwa ukisababishwa na mambo matatu ambayo ameyataja kuwa ni ugaidi wa kifikra,kiuwezo na ugaidi wa kudai haki.
Wajumbe mbalimbali wakichangia
Aidha Ameongeza kuwa dini zote duniani hakuna hata ushaidi wa dini moja ambayo inaruhusu ama kushabikia vitendo vya mauaji ya kigaidi yoyote yanayotokea afrika..
Katika hatua nyingine sheikh JALALA akizungumzia swala ambalo limekuwa likitamkwa na serikali kuwa viongozi wa dini ya kiislam wamekuwa wakiwafundisha vijana wao wa mbinu na njia za ugaidi ameitaka serikali kuacha kauli hizo kwani ni kauli za kichochezo na zisizo na ushahidi wowote na badala yake wafwatilie swala hilo kiundani pasipo kuitaja dini yoyote kuhusika.
Akizungumza katika kikao hicho muwakilishi wa wakiristo katika mkutano huo pastor PRINCE ERASTO IKONGO kutoka pentecoste Tabata amesema kuwa viongozi wa dini za kikiristo wamekuwa na hofu kubwa juu ya ndugu zao ambao ni waislam hofu ambayo wamejengewa kuwa viongozi wa dini za kiislam pamoja na waumini wao ni watu wa mauaji na ugaidi jambo ambalo amewatoa wasi wasi wakristo na kuwataka kujenga umoja na mshikamano juu ya waislam na dini zote Tanzania ili kuidumisha amani ya nchi.

Amesema kuwa hofu iliyojaa miongoni mwa viongozi wa dini za kikristo ni hofu ambayo imejengwa na wanadamu kuwa waislam ndio wanaohusika na mauaji mbalimbali ambayo yanatokea duniani ya kigaidi jambo ambalo linapaswa kufutika miongoni mwa wakristo ili waweze kudumisha umoja wanchi.

Kikao hicho kimefanyika leo Jijini Dar es salaam Ikiwa ni mwendelezo wa maadhimisho ya wiki ya ukombozi wa bara la Africa kilikua na kauli mbiu ya TUUNGANE KWA PAMOJA KUUPINGA UGAIDI AFRICA ambapo kimehudhuriwa na viongozi kutoka dini zote huku lengo kuu la kikao hicho likiwa ni kujadili kwa pamoja maswala ya ugaidi barani Africa na kuona ni njia gani zinazoweza kutumika kuondokana na tatizo hilo.

No comments: