Wednesday, July 15, 2015

HABARI PICHA--LHRC WAZINDUA KANZIDATA YA KATIBA JIJINI DAR ES SALAAM LEO


Afisa KANZIDATA wa maswala ya katiba, Mr. Majaliwa Ngairo wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu akionyesha kwa videto juu ya utumiaji wa KANZIDATA ya KATIBA kwa mgeni rasmi Mhe. Jaji mstaafu Thomas Mihayo na Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Dr. Helen Kijo-Bisimba
Afisa utafiti wa maswala ya katiba, Ms. Geline Fuko wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu akielezea juu ya utumiaji wa KANZIDATA ya KATIBA kwa mgeni rasmi na wageni waalikwa ndani ya KATIBA INFORMATION CENTRE katika ofisi za LHRC - Mbezi Upepo Avenue

Meza kuu ikiwa tayari kwa uzinduzi wa KANZIDATA ya KATIBA. Kutoka kushoto ni Dr. Khoti Kamanga, Dr. Helen Kijo-Bisimba, Mgeni rasmi Mhe. Jaji mstaafu Thomas Mihayo, Mwenyekiti wa bodi ya LHRC Prof. Geofrey Mmari na mkurungenzi wa idara ya Utetezi na Maboresho Wakili Harold Sungusia.


Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Dr. Helen Kijo-Bisimba, mgeni rasmi Mhe. Jaji mstaafu Thomas Mihayo, Mwenyekiti wa bodi ya LHRC Prof. Geofrey Mmari, Dr. Khoti Kamanga na mkurungenzi wa idara ya Utetezi na Maboresho Wakili Harold Sungusia wakifuatilia kwa umakini maelezo juu ya matumizi ya KANZIDATA (DATA BASE) ya KATIBA.

Mhe. Jaji mstaafu Thomas Mihayo akikata utepe kwa ajili ya kuizindua rasmi KATIBA INFORMATION CENTRE mapema asubui hii. 
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo Mhe. Jaji mstaafu Thomas Mihayo akiwa na Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Dr. Helen Kijo-Bisimba,wakiwa katika picha ya pamoja na washiziki mbalimbali waliopata nafasi ya kuhudhuria katika uzionduzi huo uliofanyika juijini Dar es salaam mapema leo


Muonekano wa KATIBA INFORMATION CENTRE ya kisasa kabisa katika ofisi za LHRC - Mbezi Upepo Avenue ambapo ndio uzinduzi huo umefanyika leo

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Dr. Helen Kijo-Bisimba akifungua rasmi uzinduzi wa KANZIDATA ya KATIBA

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Dr. Helen Kijo-Bisimba akiongozana na mgeni rasmi Mhe. Jaji mstaafu Thomas Mihayo, Mwenyekiti wa bodi ya LHRC Prof. Geofrey Mmari na mkurungenzi wa idara ya Utetezi na Maboresho Wakili Harold Sungusia wakielekea kuzindua KANZIDATA (DATA BASE) ya KATIBA

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Dr. Helen Kijo-Bisimba akiwa na mgeni rasmi Mhe. Jaji mstaafu Thomas Mihayo katika zoezi la Uzinduzi rasmi wa KANZIDATA (DATA BASE) ya KATIBA. 

Wageni waalikwa wakiuliza maswali mbali mbali kuhusu KANZIDATA ya KATIBA.

Kwaya ya mwalusanya ikitoa burudani katika uzinduzi huo leo

No comments: