Monday, July 27, 2015

Yametimia hapa,UKAWA wamsafisha Lowasa rasmi,Lipumba Asema anakaribishwa sana

Yale yaliyokuwa yanasemwa kuwa Mbunge wa Monduli EDWARD LOWASA atajiunga na umoja wa katiba ya wananchi ukawa sasa imekuwa rasmi baada ya umoja huo kujitokeza muda huu na kumkaribisha rasmi na kusema kuwa sasa anakaribishwa yeye pamoja na watanzania wengine kuwa wanakaribishwa kujiunga na harakati hizo.


Katika mkutano wa wanahabari uliomalizika muda huu hapa makao makuu ya chama cha wananchi CUF mkutano ambao umehudhuriwa na wenyeviti wote wa vyama hivyo wamesema kuwa sasa rasmi wanamkaribisha lowasa kujiunga na harakati zao kwani bado wanaamini ni mtu safi ambaye alichafuliwa na watanzania bado wanaimani nao japo kuwa alitemwa katika mchakato wa chama cha mapinduzi.
Nje ya makao makuu CUF muda huu
Mh mbatia anasema kuwa umoja huo lengo lake ni kuondoa mfumo uliopo ambao unaongozwa na CCM hivyo wwatafanya kila njia ambayo itasaidia kufanikisha zoezi hilo.
Maswali mengi ya wanahabari yalikuwa yakiwataka viongozi hao kuonyesha kuwa LOWASA sio fisadi kama ambavyo waliwahi kumshambulia viongozi hao wamesema kuwa kiongozi huyo sio fisadi kwani hadi sasa hana kesi yoyote mahakani ya ufisadi.

Kuhusu mgombea wa urais wa umoja huo mbatia anasema kuwa  mwanzoni mwa mwezi wa nane huku mwenyekiti wa chama cha NLD anasema kuwa hakuna ubaya kama wakimchagua mh LOWASA kugombea nafasi hiyo.
Mkutano umemalizika kwa viongozi hao kusema kuwa UKAWA iko imara na ndio tumaini jipya la watanzania na hakuna mtu wa kuivuruga.


No comments: