Saturday, August 15, 2015

CUF vs POLISI-Soma walichosema CUF muda huu kuhusu agizo la polisi juu ya kuandamana

Baada ya jeshi la Polisi nchini Tanzania kupiga marufuku maandamano ya wanasiasa wakati wa kampeni,chama cha wananchi cuf wameibuka na kusema kuwa kauli hiyo ni mzaha wa jeshi la polisi ambao unaweza kuleta madhara makubwa kwani hakuna sheria inayokataza maandamano ya wanasiasa na hawako tayari kutii sheria hiyo kwani ni uonevu wa watanzania.

Akizungumza na wanahabari mapema asubuhi leo naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho mama MAGDALENA SAKAYA amesema kuwa kuandamana ni haki ya mtanzania ya kikatiba,ambayo imeelezwa kama njia ya kujieleza,hivyo Polisi wanakiuka katiba na sheria za nchi zinazoruhusu kuandamana ambapo pia amesema wanakiuka sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 2002 ibara ya 11 ambayo inatambua maandamano na mikusanyiko kama sehemu ya shughuli za kisiasa.

Sakaya anasema kuwa ni kitu ambacho hakiwezi na hakiwezekani wakati wa kampeni kwa vyama vya siasa kufanya kampeni kimya kimya pasipo maandamano ambapo amesema ni utamaduni ambao hata nchi zilizoendelea uliwashinda huku akisema huwezi kutenganisha kuandamana na kampeni kwani ni vitu vinavyokwenda sambamba.

Aidha amesema chama cha wananchi CUF kinaona hizi ni dalili za jeshi la polisi kutumiwa na chama cha mapinduzi CCM ili kuziba aibu wanayoipata kwa kukosa umati wa watu katika mikutano yao.
Mwisho CUF wamesema kuwa hawakubaliani na agizo hilo na kusema kama polisi wataendelea na msimamo huo wao ndio watakuwa wameanzisha vurugu ambazo hazina ulazima katika uchaguzi huo.

No comments: