Monday, August 31, 2015

GLOBAL PEACE FOUNDATION, TAWI LA TANZANIA KUHAMASISHA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

 Viongozi mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Global Peace Foundation Tawi la Tanzania (GPFTZ), Martha Nghambi (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana  
wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha amani nchini Tanzania katka kipindi hiki  kuelekea uchaguzi mkuu. Kulia ni Mkurugenzi wa Baraza la Taasisi ya Viongozi wa Dini Tanzania (IRCPT), Mchungaji Thomas Goda na kushoto ni Ofisa Utawala wa GPFTZ, Hilda Ngaja.
 
 Mkurugenzi wa Baraza la Taasisi ya Viongozi wa Dini Tanzania (IRCPT), Mchungaji Thomas Goda (kushoto), akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Balozi wa Amani wa GPF, Dk.Ulimwengu.
 Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Global Peace Foundation Tawi la Tanzania (GPFTZ), Martha Nghambi (kushoto) na  Mkurugenzi wa Baraza la Taasisi ya Viongozi wa Dini Tanzania (IRCPT), Mchungaji Thomas Goda, wakionesha kipeperushi kinacho hamasisha kushiriki uchaguzi kwa amani.
 Ofisa Utawala wa Shirika hilo, Hilda Ngaja (kushoto) na Balozi wa Amani wa GPF, Dk.Ulimwengu (kulia), wakionesha kipeperushi kinacho hamasisha kushiriki uchaguzi kwa amani.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea.
Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
……………………………………………………
 Na Dotto Mwaibale
 
GLOBAL  Peace  Foundation Tawi
la  Tanzania  (GPFTZ), kwa kushirikiana  na
Mshirika  wake, Baraza  la  Wadhamini  la
Taasisi  ya  Viongozi  wa  Dini  Tanzania (IRCPT),  
wamezindua  kampeni  ya
kuhamasisha  Amani  nchini  Tanzania  katika
kipindi  hiki  kuelekea  uchaguzi  mkuu  ,
jina  la  kampe
ni  ni  “Amani Kwanza”.  
Lengo  kuu  la  kampeni hiyo  ni  kuhamasisha  watanzania  wote
kushiriki    katika  Uchaguzi  Mkuu  kwa
Amani  ambao  unatarajia  kufanyika  siku  ya
25/08/2015.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kampeni hiyo Dar es Salaam leo asubuhi, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Global Peace Foundation Tawi la Tanzania (GPFTZ), Martha Nghambi  alisema Walengwa  wakuu  wa
Kampeni  hiyo  ni  Wanawake  na  Vijana 
ambao  ni  wengi
zaidi  ukilinganisha  na  rika  na  makundi
mengine,  na  pia  Wanawake  wamekuwa
wakihathirika zaidi  endapo  inapotokea  machafuko
hali kadhalika  Vijana  wamekuwa  chanzo
        cha  uchochezi  wa
machafuko  katika  nchi  mbalimbali  duniani.
 
kampeni  hii  haina lengo  lolote  la  kuunga  mkono    ama
kupinga  Chama  chochote  cha  Kisiasa  au
mgombea  wake,  na  wala  haina  mahusiano
yoyote  ya  kisiasa na kauli k
auli  mbiu  yake ni “KURA  YANGU  UZALENDO
WANGU,  AMANI  YA  NCHI  YANGU  NI  JUKUMU
LANGU” alisema Nghambi.
Nghambi alisema Kampeni hiyo  imeandaliwa
maalumu  kwa  malengo  ya k
uwahamasisha  Wanawake
na  Vijana  kuwa  mabalozi  wazuri  wa
kulinda  na  kuitetea  Amani  ya  nchi
yetu  hasa  katika  kipindi  hiki  kuelekea  uchaguzi
Kujiepusha  na  vitendo  mbalimbali    ambavyo
vinaweza  kuchochea  uharibifu  wa  Amani
nchini Kuhamasisha  
kila  mmoja  ashiriki
uchaguzi  kwa  amani Ili  kuhakikisha.  
Alisema kampeni hiyo inafanikiwa  kutokana na Shirika  la Global  Peace kushirikiana kwa
karibu  na  vyombo  vya  habari  nchini
vikiwemo  Radio,  Luninga,  Magazeti,  na
mitandao  mbalimbali    ya  Kijamii  ikiwemo 
Twitter,  Face  Book,
instagram  na  YouTube.  
Alisema  shirika hilo ni Tawi la  Taasisi  ya  Kimataifa  isiyo ya  Kiserikali  na
isiyotengeneza  faida  Global  Peace  Foundation
(GPF)  yenye  makao  makuu  yake
Washington  DC,  nchini  Marekani.    
Alisema  shirika  hilo linahamasisha  kutetea  na  kulinda  Amani  dunia
,    shirika  hili  linaamini  ya  kuwa “ 
Kwa  Mungu  sisi
wote  ni  familia  moja” GPF  inafanya  kazi
kwa  karibu  na  mitandao  ya  kiserikali
na  watu  binafsi  katika  kuendeleza  jamii,
taifa  na  katika  kujenga  na  kulinda  misingi
na  maadili  katika  jamii  husika.
GPF  ina  rekodi nzuri  ya  kufanya  kazi  kwa  karibu  na
kwa  mafanikio  makubwa    kuhamasisha  na
kulinda  Amani  katika  nchi  mbalimbali  dunia
katika  bara  la  Afrika,  Asia,  Ulaya  na Amerika.
Kwa  upande  wa Afrika,  shirika  hili  limekuwa  likijihusisha
na  maswala  mbalimbali  ya  kijamii  katika
nchi  za  Kenya,  Uganda  na  Nigeria
kudumisha  Amani  kwenye  ukanda  wa  Afrika.

No comments: