Friday, August 21, 2015

LHRC --Waliokosa maadili wasiruhusiwe Kugombea Tena Uchaguzi wa mwaka huu

Mkurugenzi mtendaji wa Kituo cha sheria na haki za Binadam LHRC akizngumza na wanahabari leo juu ya maswala ya Maadili kwa viongozi kuelekea uchaguzi mkuu.
 Kituo cha sheria na haki za Binadamu nchini Tanzania kimeitaka Tume ya Taifa ya uchaguzi kutokupitisha majijna ya wagombea wa vyama mbalimbali ambao tayari wameshausishwa na maswala mbalimbali ya ukiukaji wa maadili ikiwemo Tuhuma mbalimbali za ufisadi, rushwa,pamoja na matumizi mabaya ya ofisi.

Akizunguimza na wanahabari mapema leo Jijini Dar es salaam mkurugenzi mtendaji wa LHRC Mama HELLEN KIJO BISIMA amesema kuwa katika kipindi hiki imeshughudiwa vyama vya siasa vikiwapitisha viongozi kuwania nyadhifa mblaimbali za uongozi huku kukiwa na viashiria vya kutoheshimu misingi ya maadili huku baadhi ya walioteuliwa wakiwa wamewahi kuhusishwa na kutajwa na kushtakiwa katika vyombo vya kikatiba kutokana na ukosefu wa maadili ya uongozi.
Amesema kuwa baadhi ya wagombea ambao wamepitishwa na vyama mbalimbali vya siasa waliwahi kuhusishwa na rushwa,matumizi mabaya ya ofisi za umma,kutowajibika,huku wengine wakiwa waliwahi kutoa kauli za kejeli zinazokinzana na kanuni za maadili ya uongozi huku wengine wakienda mbali zaidi na na kuvidharau vyombo vilivyowekwa kikatiba kusimamia maadili ya umma.

Ameongeza kuwa kutokana na viashiria hivyo ambavyo mwisho wake vinaweza kutupatia viongozi wasio na maadili ni lazima vyombo vinavyosimamia maaadili,ya viongozi wa umma kutathmini kwa makini,na kutofumbia macho viongozi wa umma ambao wanawania tena nyadhifa mbalimbali ambao walishindwa kuonyesha kiwango cha juu cha maadili wakati wa uongozi wao,ili wananchi wawe na imani nao kwa mara  nyingine.

Katika hatua nyingine mkuruhenzi huyo ameitaka taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini Tanzania kwa kuzingatia sheria ya kupambana na kudhibiti rushwa na sheria ya gharama za uchaguzi iweke na kusimamia mkakati ambao utadhibiti mianya ya rushwa na matumizi yasiyo halali ya nafasi na vyombo vya Umma katika kampeni za uchaguzi mkuu.

No comments: