Friday, August 21, 2015

Picha na Historia--Za MIAMBA nane wanaowania Urais wa Tanzania nimekuwekea hapa

Mgombea wa urais wa chama cha CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2015 Daktari John Pombe Joseph Magufuli ni mbunge wa jimbo la Chato lililoko mkoa wa Geita na ni waziri wa ujenzi wa Tanzania.

Alizaliwa tarehe 29 Oktoba 1959 wilayani Chato Mkoani Kagera. Kielimu, daktari Magufuli ana Stashahada ya elimu ya sayansi akibobea kwenye masomo ya Kemia, Hisabati. Mgombea huyo wa urais ana shahada ya umahiri wa Sayansi na shahada ya uzamivu ya kemia. Aidha daktari Magufuli amewahi kufundisha katika shule ya sekondari Sengerema miaka ya themanini kisha akajiunga na mafunzo ya JKT . Alizaliwa Oktoba 1959

Alipohitimu, daktari Magufuli na aliaanza kufanya kazi katika kiwanda cha ‘Nyanza Cooperative Union akiwa Mkemia kabla ya kuondoka hapo na kuwania ubunge.

Magufuli alianza mbio za ubunge mwaka 1995 katika jimbo la Chato na kushinda kisha akateuliwa na Rais Benjamin Mkapa kuwa naibu waziri wa Miundombinu. Katika uchaguzi wa Mwaka wa 2000 pia aligombea ubunge na kushinda na Rais Mkapa akamteua kuwa Waziri wa miundombinu.

Alianza siasa mwaka 1995 Katika uchaguzi wa mwaka 2005 daktari Magufuli aligombea ubunge kwa mara ya tatu na kupita bila kupingwa. Rais Kikwete alimteua kuongoza wizara ya Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi na baadaye akamhamishia hadi wizara ya Mifugo na uvuvi.

Mwaka 2010 alichaguliwa kuwa mbunge kwa mara ya nne na Rais Kikwete alimrudisha katika Wizara ya Miundombinu na ujenzi. Daktari Magufuli anachukuliwa kuwa ni mwanasiasa mwenye msimamo thabiti, mchapa kazi na asiye yumbishwa au hata kufuata upepo wa kisaisa.


Edward Ngoyayi Lowassa (amezaliwa 26 Agosti 1953) ni mwanasiasa nchini Tanzania.
Alichaguliwa kuwa Waziri Mkuu wa kumi wa nchi hiyo tarehe 30 Desemba 2005 akajiuzulu tarehe 7 Februari 2008 kwa kutajwa katika kamati ya bunge ya uchunguzi katika utoaji wa tenda kwa kampuni ya umeme ya Richmond kutokana nauzembe wa watendaji walio chini yake.Lowassa ni mwenyeji na alikuwa mbunge wa Monduli katika Mkoa wa Arusha.
Alisoma shahada ya kwanza 
katika mada ya tamthilia kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, halafu shahada ya pili katika sayansi ya maendeleo ya jamii kwenye Chuo Kikuu cha Hull nchini (Uingereza).
Mnamo tarehe 28 Julai 2015 alijunga rasmi na chama cha upinzani cha CHADEMA. Hiyo ni baada ya kukatwa jina lake katika kinyang'anyiro cha Urais kupitia chama tawala cha Chama cha Mapinduzi.
Siku chache baadaye aliteuliwa kuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya CHADEMA mnamo Oktoba 2015.Lowassa ni mwanasiasa mkongwe mwenye uzoefu mbalimbali katika siasa za nchini Tanzania, kwa kuwa aliwahi kushika vyeo mbalimbali katika serikali kama vile:

Waziri mdogo wa mazingira na mapambano dhidi ya umaskini katika ofisi ya Makamu wa Rais (1988-2000)
Mkurugenzi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (1989-1990)
Waziri mdogo wa haki na mambo ya bunge katika ofisi ya Makamu wa Rais (1990-1993)Mbunge wa Monduli tangu 1990

MACMILLAN LYIMO (TLP):

Macmillan Elifatio Lyimo alizaliwa tarehe 29 Januari 1964 katika kijiji cha Kondeni Matala wilaya ya Moshi Vijijini, katika jimbo la Vunjo, akiwa ni mtoto wa nne kati ya watoto sita wa familia ya mwalimu Elifatio Lyimo na mama Elingisongoya (Ametimiza miaka 51 mwezi Januari 2015).

Alianza elimu yake ya msingi katika shule za msingi Kondeni na Kirua kati ya mwaka 1975 na 1978 (darasa la kwanza hadi la nne). Kisha, mwaka 1978 hadi 1979 alisoma katika Shule ya Msingi Sanya Juu katika wilaya ya Hai . Baadaye alijiunga na Shule ya Msingi Karoro kati ya mwaka 1980 – 1981 alikomalizia darasa la saba.

Macmillan alikuwa mwanafunzi pekee aliyefaulu kutoka kwenye shule zote za kata ya Mwika kusini. Baada ya ufaulu huo wa “upweke” alichaguliwa kuendelea na masomo ya Sekondari katika Shule ya Sekondari Same mkoani Kilimanjaro akafanikiwa kuhitimu mwaka 1985.

Katika uhitimu wake wa kidato cha nne alipata Daraja la Kwanza (Division I) akachaguliwa tena kuendelea na masomo ya juu ya sekondari katika mchepuo wa ECA (Economics, Commerce na Accounts). Masomo haya ya juu ya sekondari (kidato cha tano na cha sita) aliyapata katika Shule ya Sekondari Umbwe iliyoko Moshi Vijijini (1985 - 1988) ambako nako alipata daraja la kwanza (Division I).

Baada ya hapo alijiunga na jeshi la kujenga Taifa katika kambi za Mgambo na baadaye Maramba zote zikiwa mkoani Tanga, kisha akahamishiwa makao makuu ya JKT eneo la Mlalakuwa jijini Dar es salaam, (Mwaka 1988 - 1989).

Na kisha alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuanzia mwaka 1989 na akahitimu shahada ya Biashara (Bcom) mwaka 1993. Katika kujiendeleza kitaaluma, Macmillan alijiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) mwaka 1999 – 2004 alikosoma na kutunukiwa shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Biashara (MBA). Tangu mwaka 2013 amekuwa akiendelea na masomo ya Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu Huria Tanzania na hivi sasa yuko katika hatua ya utafiti akitarajia kuhitimu shahada hiyo ya falsafa miaka michache ijayo.

Tangu ahitimu shahada yake ya Biashara, Macmillan hajawahi kuajiriwa serikalini na haamini katika “kuajiriwa na serikali”. Amefanya shughuli za biashara ndogo ndogo kabla ya kufungua kampuni yake binafsi inayojihusisha na masuala ya madini na raslimali za Nchi.

Amejishughulisha sana na utafiti juu ya utajiri wa madini katika nchi hii pamoja na raslimali zingine. Lyimo amenieleza kuwa, Utafiti huu wa zaidi ya miaka 15 umemwezesha kujua ni kwa kiasi gani taifa hili ni tajiri katika eneo la madini,mafuta , gesi, ardhi, maji, mito na maziwa.

Ndoto yake kubwa ni kuona namna gani taifa linaweza kunufaishwa na rasilimali zake. Muda mfupi nilioongea nae tayari alishanipa vionjo vya kampeni yake mwezi oktoba mwaka huu vikiongozwa na kauli mbiu “FUTA UMASIKINI TANZANIA”!

Macmillan ni mwandishi mzuri wa vitabu na kitabu alichokikamilisha hivi karibuni kikiwa na kurasa zaidi ya 200 kinaitwa “Nuru ya Mabadiliko Tanzania kutokea mwaka 2005” ambacho kiko kwenye hatua za uchapishwaji.

Mwanasiasa huyu hapendi kuongea masuala yake ya kifamilia kwa hiyo sikupata taarifa za hali ya ndoa yake.
Chifu Lutalosa Yemba (ADC) ni mgombea wa chama hicho chenya maskani yake Buguruni jijini Dar es salaam,YEMBA pia alikuwa mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Shinyanga .kabla ya kutimuliwa ndani ya chama hicho mapema mwaka huu na kujiunga na chama cha ADC na sasa ndiye mgombea urais wa chama hicho




Fahmi Nasoro Dovutwa ni Mwenyekiti wa kitaifa wa Chama cha United Peoples Democratic Party (UPDP). Alizaliwa Februari 27, 1957 mjini Kisarawe mkoani Pwani (Amefikisha miaka 58 Februari mwaka huu).

Dovutwa alianza elimu yake ya msingi mwaka 1967 katika shule ya msingi Zanaki hadi alipohitimu mwaka 1974 alipoendelea na masomo ya sekondari katika shule ya sekondari Azania ambako alihitimu mwaka 1977.

Rekodi za elimu za Dovutwa zimekuwa “kizungumkuti” kupatikana. Hata taarifa zake binafsi alizotoa kwa ajili ya rekodi za Bunge Maalum la Katiba zinasisitiza kuwa ameishia kidato cha nne.

Juhudi za kumpata yeye mwenyewe ili akamilishe rekodi zake hazikufua dafu na ni yeye peke yake tangu nianze kufanya uchambuzi wa watu wanaotajwa kuwania urais, ambaye hakutoa ushirikiano kabisa ili kunifanya nipate rekodi zake sahihi. Hata hivyo hilo haliwezi kunizuia kumchambua.

Watu wa karibu yake wamenijulisha kuwa kwa muda mrefu amekuwa akijishughulisha na kazi za ujasiriamali katika soko la Magereza jijini Dar es Salaam hadi baadaye alipochaguliwa kuongoza chama cha UPDP ambacho yeye ni mwenyekiti hadi sasa.

Mwaka 2014, alikuwa ni miongoni mwa Watanzania waliopata fursa ya kuteuliwa na Rais wa Tanzania kupitia kundi la vyama vya siasa, na kuwa mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba lililofanya kazi yake mjini Dodoma na kukamilisha Katiba Inayopendekezwa ambayo hata hivyo imeligawa taifa katika vipande viwili. Dovutwa ameoa na ana watoto.
Mbio za ubunge

Katika historia ya kisiasa ya Dovutwa, hakutoa pia rekodi zinazoonyesha kama aliwahi kugombea ubunge katika jimbo lolote na hata nilipozitafuta sikufanikiwa kuzipata.
Mbio za urais

Kiongozi huyu alijitosa katika mbio za urais mwaka 2010 akitumia tiketi ya chama chake cha UPDP. Katika uchaguzi ule ambao Jakaya Mrisho Kikwete aliongoza kwa ushindi wa asilimia 62.83, akifuatiwa na Willibroad Slaa aliyekuwa na ushindi wa asilimia 27.5, na Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF akiwa na asilimia 8.28, Dovutwa aliibuka katika nafasi ya mwisho akiwa na asilimia 0.16 ya kura zote kwa kupitwa na Peter Mziray wa APPT (asilimia 1.15), Hashim Rungwe wa NCCR (asilimia 0.31), na Mutamwega Bhatt wa TLP aliyekuwa na asilimia 0.21 ya kura zote.

Katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu, Dovutwa hajatangaza popote kuwa atagombea tena nafasi ya urais lakini duru za kisiasa ndani ya chama hicho ikiwamo kutoka kwa baadhi ya viongozi waandamizi, zimenieleza kuwa anapewa nafasi kubwa ya kugombea tena.


Hashim Rungwe Spunda, ni Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania akifanya kazi zake kama wakili binafsi. Alizaliwa tarehe 01 Januari 1949 katika eneo la Ujiji, mkoani Kigoma (Ametimiza miaka 66 mwezi Januari mwaka huu).

Hashim alianza elimu ya msingi katika shule ya msingi Kipampa iliyoko mkoani Kigoma kati ya mwaka 1959 – 1966 na akajiunga na masomo ya sekondari katika Shule ya Sekondari ya Chuo Kikuu cha Cambridge kati ya mwaka 1967 – 1969 na kuhitimu kidato cha nne, kabla ya kuendelea na masomo ya kidato cha tano na sita hapa hapa Tanzania.

Mwaka 1975 alisoma ngazi ya Cheti katika Taasisi ya Kukuza Mauzo (Tafsiri yangu) ya Dar Es Salaam, mwaka 1977 alisoma Lugha ya Kifaransa kwa ngazi ya cheti katika taasisi ya “Alliance Francais” ya jijini Dar Es Salaam na kisha akasoma lugha ya kiarabu na elimu ya dini ya kiislamu kwa ngazi ya shahada katika Chuo Kikuu cha Mfalme Abdul kilichoko Saudi Arabia kati ya mwaka 1979 – 1982.

Mwaka 1989 – 1989 alisoma Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam ngazi ya Cheti, akichukua masomo ya Usimamizi wa Umma lakini pia mwaka 1991 alisoma ngazi ya cheti hapo hapo Chuo Kikuu, akijikita katika eneo la Historia ya Afrika na Falsafa ya Historia na Masuala ya Maendeleo (Tafsiri yangu).

Hashim aliendelea zaidi kielimu alipoamua kubobea katika sheria, alijiunga na Chuo Kikuu Huria Tanzania na kusoma shahada ya sheria kuanzia mwaka 1996 na kuhitimu mwaka 2003 na mwaka huohuo 2003 akasajiliwa kuwa wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Kwa upande wa ajira, Hashim amefanya kazi na mashirika mbalimbali ya ndani ya nchi. Kwa mfano, kuanzia mwaka 1969 hadi 1973 amekuwa ni Ofisa aliyeajiriwa serikalini na kufanya kazi katika idara mbalimbali za sekta ya umma.

Pia, mwaka 1982 hadi leo amekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Udalali ya Bahari, lakini pia kuanzia mwaka 1990 hadi leo amejiajiri katika kampuni ya Bahari Motors inayojishughuliza na uuzaji wa magari akiwa kama Mkurugenzi Mtendaji

Kisiasa, Hashim aliwahi kuwa mwanachama imara wa TANU kati ya mwaka 1966- 1977 na kisha CCM kati ya mwaka 1977 – 1995. Ndiyo kusema kuwa wakati mfumo vyama vingi unaanzishwa mwaka 1992 yeye alikuwa mwanachama wa CCM kwa miaka mitatu zaidi kabla ya kuhamia NCCR Mageuzi mwaka 1996.

Alipokuwa NCCR alishiriki hatua mbalimbali za chama hicho katika kupigania mabadiliko, lakini alijiondoa NCCR mwaka 2012 na kuanzisha chama cha siasa kinachojulikana kama CHAMA CHA UKOMBOZI WA UMMA (CHAUMMA) na baada ya kuanzisha chama hicho alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kitaifa wa CHAUMMA mwaka 2014 na anashikilia wadhifa huo hadi hivi sasa.
Hashim Rungwe ameoa na ana watoto watano.
ANNA MGHWIRA kutoka ACT kusomea shahada ya Sheria. Kati ya mwaka 1987 - 1998, aliendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa, akifanya kazi ndani na nje ya nchi na kupata uzoefu mkubwa.

Safari ya elimu ya Mghwira ilikamilikia Chuo Kikuu cha Essex, Uingereza ambako alianza Shahada ya Uzamili ya Sheria (LLM) mwaka 1999 na kutunukiwa mwaka 2000. Licha ya kuwa mwanasheria na mtheologia aliyebobea, pia amefanya kazi za maendeleo kwa muda mrefu na ana uzoefu katika uendeshaji wa Serikali za Mitaa, utumishi katika mashirika ya kimataifa, kitaifa na mashirika ya dini ambamo amejihusisha na masuala ya wanawake, watoto, wakimbizi, utawala na haki za binadamu.

Mghwira ana historia ya kupenda siasa, masuala ya jamii na michakato ya maendeleo kama inavyojidhihirisha katika maandiko yake mbalimbali katika majarida na magazeti ya hapa ndani ya nchi. Alianza siasa tangu wakati wa Tanu akiwa mwanachama wa Umoja wa Vijana wa Tanu (Tanu Youth League) na aliwahi kushinda tuzo mbalimbali kutokana na ushiriki wa juu katika Tanu lakini baadaye ilipoanzishwa CCM alipunguza ushiriki wake ili ajipe muda katika masomo na baadaye ndoa na malezi ya watoto.

Kwa kipindi kirefu, hakuwa anajihusisha na siasa hadi alivyoamua kujiunga na Chadema mwaka 2009 ambako alishika nafasi mbili tu za uenyekiti wa baraza la wanawake ngazi ya wilaya na katibu wa baraza la wanawake mkoa


MGOMBEA WA MWISHO NI Janken Kasambala (NRA)ambaye bado tunatafuta picha na historia yake

No comments: