Thursday, August 20, 2015

STARS KWENDA UTURUKI MOJA KWA MOJA


Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro sasa itaondoka nchini siku ya jumapili usiku kuelekea Istambul nchini Uturuki kwa kambi ya siku nane kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria Septemba 05, 2015.

Awali Taifa Stars ilikua ipitie Muscat nchini Oman kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya nchi hiyo, lakini kutokana na shirkikisho la Soka la Oman kushindwa kukidhi mahitaji ya Kanuni za FIFA za uuandaaji wa mechi ya kimataifa ya kirafiki sasa mchezo huo hautakuwepo tena.
Stars inatarajiwa kuondoka jumapili usiku na shirika la ndege la Uturuki (Turkish Airlines) na kuwasili Istambul (Ataturk Airport) siku ya jumatatu majira ya saa 5 kamili asubuhi, kisha kuelekea Kocael katika hoteli ya Green Park Kartepe ambapo ndio itakua kambi yake ya wiki moja.
UCHAGUZI WA TEFA WAAHIRISHWA
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kupitia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Aloyce Komba imeitisha majalada ya kamati ya uchaguzi ya TEFA na kamati ya uchaguzi ya DRFA baada ya kupokea malalamiko na rufaa kutoka kwa wagombea.
Kamati ya Uchaguz ya TFF imeyaomba majalada hayo ili ijiridhishe na kuona haki inatendeka kwa wagombea wote na baadae tarehe mpya ya uchaguzi itatolewa.
SAANYA KUCHEZESHA AZAM NA YANGA
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limemteua mwamuzi wa kati Martin Saanya kuchezesha mchezo wa Ngao ya Jamii jumamosi, badala ya mwamuzi Israle Nkongo aliyekua amepangwa awali.
Mwamuzi Israel Nkongo anasumbuliwa na matatizo ya misuli ya paja, ambayo itampelekea kukaa nje ya uwanja kwa takribani siku kumi, hali iliyopeleka TFF kumbadilisha mwamuzi huyo kuelekea kwenye mchezo huo wa jumamosi.

No comments: