Thursday, August 20, 2015

Mambo matatu ambayo MBATIA amewaambia wanahabari jioni hii




















Wakati Umoja wa Katiba ya wananchi UKAWA ukikumbwa na changamoto ya ugawanaji wa majimbo baada ya maeneo mengi nchini Tanzania kuibuka migogoro mara baada ya majimbo ya uchaguzi kugawanywa kwa vyama hivyo,hatimaye mwenyekiti wa chama cha NCCR MAGEUZI ambaye ni mwenyekiti mwenza wa umoja huo ameibuka na kutoa onyo kali kwa viongozi ambao wanakuwa wabinafsi wa kutokutaka kuachiana majimbo na kusema kuwa ubinafsi ni jambo ambalo halitaendekezwa ndani ya umoja huo.

Akizungumza na wanahabari leo jioni hii Dar es salaam amesema kuwa mara baada ya kukamilika kwa kazi ya kugawana majimbo kwa vyama vinne vinavyounda umoja huo kumeibuka sintofahamu ya baadhi ya watu kungangania majimbo ambayo tayari wamepewa watu wengine jambo ambalo amesema kuwa sio makubaliano ya umoja huo na hawatavumilia viongozi wa namna hiyo.

Amesema kuwa moja ya maazimio makubwa ya umoja huo ni kuepuka ubinafsi na kuhakikishya kuwa mambo wanayoyahubiri kwa wananchi wanayatekeleza kwa vitendo ikiwa ni pamoja na amani na umoja hivyo hawako tayari kuona chama au mtu yoyote anaanzisha vurugu ndani ya umoja huo.

Amesema Tayari leo jioni viongozi wakuu watakutana kuona ni jinsi gani wanaweza kushughulikia jambo hilo ili ndoto za watanzania za kuhakikisha kuwa wanauondoa mfumo dhalimu wa CCM uliopo kwa sasa zinatimia na nchi inakuwa na amani na utulivu mkubwa.

KUHUSU STORY YA CHAMA CHAKE KUJITOA UKAWA

Akizngumzia sakata hilo ameonyeshwa kushangazwa na taarifa hizo huku akisema kuwa atakuwa ni kichaa kama mtu aliyeasisi mageuzi nchini Tanzania anaweza kuyakimbia kipindi ambacho mageuzi yanazaa matunda mazuri.

Amesema kuwa UKAWA ni zao la NCCR mageuzi kwa kuwa lengo kuu la ukawa sasa ni kufanya mageuzi ya mfumo uliopo sasa na kuweka mfumo ambao ni rafiki kwa wananchi hivyo hana mpango na hawezi hata siku moja kujitoa katika umoja huo na story zinazoenea ni muendelezo wa mbinu chafu za wapinzani za kujaribu kuwagombanisha ndani ya umoja huo jambo ambalo amesema  wamechelewa kulifanya.

KUHUSU KUPIGWA MARUFUKU KUTUMIA UWANJA WA TAIFA KUZINDUA KAMPENI.
Mbatia akizungumza kwa mshangao mkubwa amesema kuwa hajaona sababu ya msingi na ya uhakika ya kuzuiliwa kufanya shughuli zake ndani ya uwanja wa taifa ambao ulijengwa na kodi ya watanzania huku akisema kuwa yote hii ni kutokana na serikali kumaliza sehemu zote za wazi kwa kuwauzia watu na sasa watanzania hawana hata mahali pa kukutana na kujadili mambo yao wakiwa na amani.

Pamoja na katazo hilo la serikali MBATIA amesema kuwa haliwezi kuwazuia kukutana na watanzania hivyo leo jioni watajadili kwa pamoja na kupata majibu kuwa ni wapi na lini wanaweza kuzindua kampeni zao kwa kumnadi mgombea wake wa nafasi ya urais

No comments: