Saturday, September 12, 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA KUKAGUA NA KUKABIDHI MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA WA CHWAKA, UNGUJA

1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Chwaka, Unguja, wakati alipofika kutembelea kukagua na kukabidhi Mradi wa Maji safi na salama wa Chwaka, leo Sept 12, 2015.
Picha zote na OMR
2
Baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Chwaka na Viongozi, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akiwahutubia alipofika kijijini hapo leo Sept 12, 2015 kwa ajili ya kutembelea kukagu na kukabidhi mradi wa maji safi na salama wa Chwaka.
3
Msimamizi wa Mradi wa Maji safi na salama wa Chwaka, Malcom Nyanda, akizungumza kuelezea changamoto za mradi huo wakati wa hafla hiyo ya makabidhiano ya mradi.

4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Fundi mkuu wa Tanki la maji, Yohana Mkoloma, wakati alipotembelea kukagua Mradi wa Maji safi na Salama wa Chwaka, Unguja leo Sept 12, 2015.
5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Msimamizi wa Mradi wa Maji safi na salama, Malcom Nyanda, wakati alipotembelea kukagua na kukabidhi Mradi huo wa Maji safi na Salama wa Chwaka, Unguja leo Sept 12, 2015.
67
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoka kukagua mradi wa Maji safi na salama baada ya kukabidhi mradi huo kwa Kamati ya Maendeleo ya Kijiji cha Chwaka, leo Sept 12, 2015.
8
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya viongozi wa Kijiji cha Chwaka baada ya kutembelea kukagua na kukabidhi mradi ya Maji safi na salama wa Chwaka, leo Sept 12, 2015 Unguja

No comments: