Saturday, September 12, 2015

RADIO 5 wajichimbia Dar es salaam kusaka vipaji Mtaani,Tizama walichokifanya Hapa

Wasanii mbalimbali ambao ni vijana wenye vipaji waliojitokeza katika viwanja vya TP SINZA Jijini Dar es salaam kuonyesha vipaji vyao katika mchakato wa RADIO 5 KAMATA KIPAJI wenye lengo la kusaka vijana wenye vipaji na kuwainua kutokana na vipaji vyao(PICHA ZOTE NA EXAUD MSAKA HABARI)
 Na Exaud Msaka Habari
Katika kuonyesha kuwa wapo karibu na vijana wa kitanzania katika kuwasaidia kuwainua kiuchumi na kiuwezo,kituo cha Radio maarufu kutoka kaskazini mwa Tanzania ARUSHA Radio   5 kimenzisha mchato maalum  wa kusaka vipaji kwa vijana wa kitanzania mchakato ambao umeanzia Jijini Dar es salaam ukiwa na lengo la kuhakikisha kuwa wanamuwezesha kijana mwenye kipaji kufikia malengo na ndoto zake
Radio 5 imekuwa na michakato mbalimbali ili kusaidia vijana katika secta tofauti tofauti zinazohusu  maisha yao ya kiuchumi huku ikiwa inawaunga mkono vijana wenye shughuli mbalimbali ambao hufika radioni hapo kuomba saport ikiwa ni pamoja na vijana wa sarakasi,ujasiriamali na fani nyingine.


Mchakato ambao sasa unatajwa kuwa utakuwa msaada mkubwa kwa vijana ambao umezinduliwa Jijini Dar es salaam na kupewa jina la RADIO 5 KAMATA KIPAJI katika viwanja vya TP sinza darajani ilishughudiwa vijana wengi wakijitokeza kuonyesha vipaji vyao ili waweze kuibuka na zawadi mbalimbali ambazo zinatolewa na waandaji hao.
Katika zoezi hilo vijana walitakiwa kutuma nyimbo zao radioni ikiwa ni pamoja na kujiandikisha majina yao ili siku waandaaji hao watakapofika katika mtaa waliopo basi waweze kupata nafasi ya kuonyesha vipaji vyao,na kupatikana washindi ambapo mchakato huo utapita katika maeneo yote ya jiji la Dar es salaam na mwisho kuwapata washindi wanne ambao ndio watakaoibuka na zawadi kabambe.


Lengo kuu la mchakato huo ni kuwasaka vijana ambao wanavipaji na wapo mtaani kutokana na sababu mbalimbali ambazo wameshindwa kuonyesha vipaji hivyo ambapo RADIO 5 wameamua kupita katika mitaa hiyo kuhakikisha kuwa vijana hao wanapata nafasi ya kuonyesha vipaji walivyo navyo kwa watanzania.
Msaanii maarufu wa music wa Uswazi Msaga Sumu maarufu kama Mfalme wa mtaani akitoa burudani wakati wa mchakato huo uliofanyika jijini Dar es salaam 
Wakati zoezi hilo likiendelea mtandao huu ulipata nafasi ya kuzngumza na mkurugenzi wa RADIO 5 Bw ROBERT FRANCIS ambaye amesema kuwa ni jambo jema kuona kazi hilo imeanza kwa amani na furaha hivyo watanzania waendelee kuwaunga mkono huku akiwataka vijana mbalimbali wenye vipaji mkoani Dar es salaam kuendelea kujitokeza maeneo mbalimbali ambapo ziezi hilo litakuwa linafanyika pamoja na kuendelea kusikiliza Radio hiyo.

Naye meneja vipindi wa RADIO 5 Ndugu MATHEW PHILIP Akizungumza na mtaandao huu wakati zoezi hilo likiendelea amesema kuwa kupitia vipindi vya Radio hiyo hasa vipindi vya kutafuta vipaji nyumba kwa nyumba Dar es salaam vijana wataweza kuinua vipato vyao huku akisisitiza kuwa watanzania waendelee kusikiliza RADIO 5 kwani kuna mambo mengi na mazuri yanaendelea kuwajia.
Umati wa watanzania waliojitokeza kushugudia vipaji vikionyesha uwezo Jukwaani
Meneja biashara wa kituo hicho cha Radio Bi ANGELA MAINA alisema kuwa maana halisi ya kufanya zoezi hilo ni kuwapa vijana nafasi ili kukuza vipaji vyao hasa katika tasnia ya music ili miaka ijayo watanzania waone matunda ya kazi hiyo haswa kwa washiriki wa zoezi hilo.

Aidha meneja masoko na mahusiano wa RADIO 5 Bi SARAH LAZARO alisema kuwa pamoja na lengo kuu la mchakato huo ni  kuvumbua na kunyanyua vipaji lakini pia ni nafasi kwa wadau wa biashara na mashirika binafsi haswa yanayojihusisha na maswala ya kijamii kuanza sasa kushirikiana na radio 5 ili kukuza biashara zao na kushiriki katika kuendeleza jamii.
Timu nzima ya watangazaji pamoja na wafanyakazi wa Radio 5 ambao ndio wanaoendesha mchakato huo wa RADIO 5 KAMATA KIPAJI unaoendelea jijini Dar es salaam wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kazi hiyo kumalizika kwa siku ya kwanza
Katika mchakato huo endelevu utakao fanyika katika jiji la Dar es salaam unataraji kuwapata washindi wanne wa mkoa huu ambapo washindi hao watajinyakulia zawadi mbalimbali kama ifuatavyo

Mshindi wa kwanza anataraji zawadi ya kurekord albam nzima bure kwenye studio za kisasa na kupata promotion kubwa ya kazi yake,mshindi wa pili anataraji kurekord nyimbo mbili bure pamoja na pamoja na promotion ya miezi sita(6),mshindi wa tatu atapata kurekord nyimbo moja pamoja na promotion ya miezi mitatu,huku mshindi wan ne ataweza kurecord nyimbo moja pamoja na promotion ya mwezi mmoja.

IMEANDALIWA NA EXAUD MSAKA HABARI-HABARI24 BLOG
Picha zaidi nimekuwekea hapo chini

















No comments: