Wednesday, September 9, 2015

Tigo na DTBi wazindua huduma ya kurejesha kumbukumbu na kuzuia wizi simu za mkononi


 Kampuni ya simu ya Tigo Tanzania kwa kushirikiana na Dar es Salaam Teknohama Business Incubator (DTBi) leo wamezindua huduma inayowawezesha watumiaji wa simu za kisasa za mkononi (smartphone) kurejesha kumbukumbu na kupatikana iwapo simu itapotea au kuibiwa.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez alisema, 

“Kama kampuni iliyoko msitari wa mbele katika kuleta mabadiliko ya kidigitali nchini, huduma hii mpya iitwayo Tigo Backup itawawezesha wateja wa Tigo kurejesha orodha ya majina kwenye simu, picha, video, ujumbe mfupi (SMS) na vitu vingine vilivyopotea, kuibiwa au kutokana na ubovu wa simu. Wateja wataweza pia kugundua na kurejesha simu zao zilizopotea au kuibiwa.”




Akielezea huduma hiyo ya kama ya kipekee, Gutierrez alisema Tigo Backup inamuwezesha mteja aliyepoteza simu yake kuwa na uwezo wa kupata picha ya aliyemwibia kwani simu itapiga king’ora, kuonyesha simu hiyo ilipo, simu itajifunga ili kuzuia matumizi mabaya, kumjulisha mwenye simu pindi abadilishapo laini ya simu na pindi simu inapopoteza habari muhimu. Huduma ya Tigo Backup imebuniwa na mwanafunzi  mzawa kutoka DTBi. 

Alisema sifa zote hizi zitawezeshwa kupitia ujumbe mfupi (SMS) au kupitia wavuti ya: https://www.tigobackup.com.” Alisema kuwa huduma hii ya kurejesha taarifa, ‘Tigo Back up’ itamgharimu mteja Tsh. 500/= kwa mwezi ilhali huduma nyingine kama vile kurejesha kumbukumbu ya orodha ya majina kwenye simu, taarifa ya kubadilisha laini ya simu na huduma ya kufunga simu iliyoibiwa zitatolewa bure. Aliongeza kwamba wateja wategemee huduma nzuri kutoka kwa Tigo huduma kwa wateja kutokana na huduma hii mpya itakayowawezesha kupata ulinzi mzuri dhidi ya wizi wa simu zao.    

Sifa tofauti zaidi kutokana na huduma hii ya kurejesha kumbukumbu ya usalama yaani Tigo Backup, ni kwamba mtu hahitaji kuunganishwa na intaneti ili kupata huduma hio. Mtu anaweza tu kufuatilia bure simu iliyopotea au kuibiwa, mahali na taarifa za mtu anayetumia simu hiyo. Huduma hii itapatikana kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza kwaajili ya matumizi ya Watanzania wote kwa ujumla.    
                                                                 
Hafla ya uzinduzi huo ilihudhuriwa na  Waziri wa Mazingiri dkt.Binilith Mahenge aliyesisitiza kuwa jitihada zza serikali kuendelea kujenga mazingira mazuri ili kusaidia ukuaji wa tasnia ya tehama na kuifanya iwe na mchango mkubwa kwa kipato taifa na kutoa ajira nyingi kwa vijana.

“Lengo letu ni kuendeleza kundi kubwa la rasilimali watu la TEHAMA, ikiwa ni pamoja na ubunifu wa programu za kwenye kompyuta katika ngazi zote ili kuziba pengo la kidijitali (vijijini na mijini)”, alisema Dkt.Mahenge.

Kwa upande wake  Mhandisi George Mulamula ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi alisema kuwa Tigo Backup ni matokeo ya ushiriakiano baina ya kampuni ya Tigo Tanzania na DTBi wakiwa na lengo la kukuza na kuendeleza huduma za kidigitali kama chachu ya maendeleo kwa jamii.

“DTBi imeendeleza kampuni ya Magilatech ambayo ni kampuni ya habari na mawasiliano inayoendeshwa na vijana wa Tanzania.” Aliwashukuru Tigo kwa kuwa na malengo sawa na DTBi la kuendeleza vijana na wanawake wa Tanzania katika kuwaandalia mbinu za kupambana na kuondokana na matatizo ya kijamii kwa kuwaandalia nafasi za kazi nchini. 


Akifafanua kuhusu huduma hiyo ya Tigo Backup kuwa na uwezo wa kurejesha kumbukumbu ya simu, “Ili kupata huduma hii, mtu anatakiwa kuwa na laini au namba ya Tigo iliyosajiliwa na simu ya kisasa yenye mfumo wa android, kuihifadhi kwenye simu yake kutoka kwenye Playstore na usajili kufuata kwa kuingiza namba yake ya simu, neno siri na anwani ya wavuti,” Huduma hii itapatikana kwa watumiaji wa simu za kisasa zenye mfumo wa android kwanza na kisha baadaye kwa wale watumiaji wa simu zenye mfumo wa IOS.    


No comments: