Wednesday, September 30, 2015

TOROKA UENDEEE--Sasa ni Kesho Dar es salaam,wote mnakaribishwa huko



Kama utakuwa na kumbukumbu nzuri ni kuwa jana tumekurepotia habari za uzinduzi wa kampeni mpya ya mgombea wa chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA iliyopewa jina la TORIKA UJE ambayo ilipangwa kuzinduliwa leo Jijini Dar es salaam,Habari za ndani zinaeleza kuwa Watanzania wengi wamekuwa na maombi ya jinsi ya kufika kwenye shughuli hiyo jambpo ambalo limewalazimu waandaaji wa Tukio hilo kulifanya katika maeneo ya wazi ili watanzania wengi waweze kulishughudia.Habari za ndani ambazo tunazo sasa ni kuwa alhamis ndio tukio hilo litafanyika na hii ni moja ya Taarifa ambazo tunazo unaweza kupitia na kushare na wengine



Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kinakualika katika mkutano wa mgombea Urais kupitia vyama vinavyounda ukawa mh. Edward Ngayai Lowassa utakaofanyika alhamisi ya tarehe 1 october katika viwanja vya tanganyika pekas kawe kuanzia saa nane mchana wakazi wote wa jiji la Dar es salaam na maeneo jirani mnakaribishwa UKAWA tumaini letu..

No comments: