Thursday, October 15, 2015

Habari na Video--TACCEO WATOA KASORO ZIIZOKUWEPO WAKATI WA UANDIKISHWAJI BVR

Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC Bi HELLEN KIJO BISIMBA akifafanua jambo mbele ya wanahabari baada ya kuwasilishwa kwa report nzima ya TACCEO juu ya mchakato wa uandikishwaji wa wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo mpya wa BVR
 Na Exaud Msaka habari
Mtandao wa asasi za kiraia wa kiuangalia chaguzi nnchini Tanzania TACCEO leo umetoa report yake ya zoezi la uandikishwaji wa daftari la kudumu la wapoga kura lakwa mfumo mpya wa kielectronic BVR huku wakionyesha kutokuridhiswa na jinsi zoezi hilo lilivyoendeshwa na kutaja baadhi ya kasoro zilizofanya zoezi hili kutofanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam Mkurugenzi mtendaji wa Kituo cha sheria na haki za Binadamu nchini ambao ndio waratibu wakuu wa mtandao huo DK HELLEN KIJO BISIMBA amesema kuwa pamoja na tume ya uchaguzi kusema kuwa zoezi hilo lilifanikiwa lakini mchakato huo ulikumbwa na kasoro nyingi.
Mwenyekiti wa mtandao wa Asasi za kiraia wa kuangalia chaguzi nchini TACCEO Bi MARTINA KABISAMA akifafanua jambo kwa wanahabari mapema leo
Akizitaja kasoro moja wapo iliyokuwa kikwazo kikubwa katika mchakato wa uandikiswaji ni kukosekana kwa elimu mahususi ya mpiga kura juu ya zoezi la auandikishwaji na umuhimu wa zoezi lenyewe jambo ambalo amesema kuwa limekuwa ni kikwazo kikubwa kwani wananchi wengi walikuwa hawaelewi nini maana ya mchakato huo huku wengine wakiwa hawataki hata kujiandikisha kwa kuhofia kuwa kuna mbinu mbalimbali zinatumika ili kupata taarifa zao.


Amesema kuwa maeneo mengi kulikuwa na usumbufu mkubwa wa wananchi kaumini kwa mashine zile zilikuwa na madhara kwa afya zao,wengine wakiamini kuwa wanapimwa virusi vya ukumwi bila kujijua huku wengine wakiamini kuwa zoezi lile ni maswala ya kishirikina yakihusishwa pia na imani za kishetani za Fremason huku wengine wakiamini kuwa wakiwa na vitambulisho vile vya awali haikuwa na haja ya kujiandikisha upya, jambo ambalo amesema kuwa yote hayo ni kutokana na kukosekana kwa elimu ya mpiga kure kipindi cha zoezi la uandikishwaji.

Makamu mwenyekiti wa TACCEO Bwana ISRAEL ILUNDE akifafanua mambo kadhaa ambayo mtandao huo uliyashughudia wakati wa zoezi la uandikishwaji
Chanagamaoto nyingine ambayo TACCEO wamekiri kukutana nayo wakati wa zoezi hilo ni waandikishaji wa zoezi hilo ikiwa  na maana ya mawakala waliopewa kazi ya kuandikisha kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya matumizi ya mfumo huo pamoja na mashine husika jambo ambalo wamesema kuwa lilikuwa ni changamoto kubwa kwa wafanyakazi hao na kusababisha zoezi hilo kwenda kwa kusua sua hali ambayo wamedai ilijitokeza katika kila eneo nchini Tanzania.


Dk HELLEN KIJO BISIMBA amesema kuwa changamoto nyingine ambazo zilikuwa zikiukumba mchakato huo ni pamoja na ubovu wa mashine ambao ulisababisha zoezi kuahirishwa mara kwa mara,wanafunzi kukosa haki yao ya kujiandikisha,pamoja na matatizo ya kiuhakiki ambapo watu waliokuwa hawapati nafasi ya kuhakiki taarifa zao kabla ya kupewa kitambulisho jambo ambalo limesababisha watu wengi kupewa vitambulisho ambavyo vina taarifa ambazo sio za kweli.
Wadau
Akizungumza na wanahabari mwenyekiti wa TACCEO Bi MARTINA KABISAMA amesema kuwa ni lazima tume ihakikishe kuwa inarekebisha kasoro zilizojitokeza katika mchakato wa uandikishwaji wa BVR ili usijirudie tena wakati wa uchaguzi jambo ambalo litasaidia uchaguzi kuwa wa huru na haki kwa watanzania wote.VIDEO IPO CHINI

No comments: