Thursday, October 15, 2015

Tigo Yampokea Msanii Diamond, Umati mkubwa wafurika kumlaki jijini Dar.

Msanii Diamond Platnumz akiongea na waandishi wa habari na mashabiki waliojitokeza kumpokea  mara baada ya kuwasili kutoka nchini Marekani alikopokea Tuzo za Afrimma. Wengine kushoto kwake Meneja wake Babu Tale, Meneja wa Tigo music Hamza Balla, na Mtaalam wa mitandao ya kijamii toka Tigo Samira Baamar.


Msanii Nassib Abdul Diamond (katikati), Meneja wa Tigo music Hamza Balla (kushoto) na Mtaalam wa mitandao ya kijamii toka Tigo Samira Baamar wakiwa kwenye picha ya pamoja kuwaonyesha mashabiki tuzo alizonyakua za Afrimma.


Msanii Diamond( kulia) akiwa na mama yake na Meneja wake wa kimataifa.



Msanii Queen Darlin akipeperusha bendera juu ya Lori kumfagilia kaka yake Diamond.


Meneja wa Tigo music, Hamza Balla akiongea na waandishi wa habari na mashabiki waliojitokeza kwa wingi kumpokea msanii wa kizazi kipya Nassib Abdul Diamond (kushoto)mara baada ya kuwasili kutoka nchini Marekani alikopokea Tuzo za Afrimma. Pembeni kulia Mtaalam wa mitandao ya kijamii toka Tigo Samira Baamar.

No comments: