Tuesday, October 13, 2015

LHRC WATOA MAFUNZO KWA WAGOMBEA WANAWAKE WA UBUNGE NA UDIWANI NCHINI TANZANIA

Mgombea ubunge wa ubungo kwa tiketi ya chama cha TLP Mama GODLIVA MANUMBA na kulia kwake ni  mgombea ubunge wa jimbo la ubungo kwa tiketi ya ACT-wazalendo Mama NYANJURA NYARINDO wakizngumza na wanahabari wakati wa mafunzo hayo ambayo yamefanyika kwa siku mbili Jijini Dar es salaam
 Wagombea wa nafasi za udiwani na ubunge ambao ni wanawake katika uchaguzi mkuu wameomba vyombo vya habari pamoja na wadau wa uchaguzi nchini kuwapa kipaumbele katika nyakati hizi za kampeni kutokana na kile walichodai kusahaulika na kipaumbele kikubwa kupewa wagombea wanaume katika uchaguzi wa mwaka huu.
Wagombea mbalimbali walioshiriki katika mafunzo hayo wakichangia mada katika mafunzo hayo
Wito huu umetolewa leo jijini Dar es salaam wakati wa mafunzo kwa wagombea wa nafasi hizo wanawake nchini Tanzania mafunzo ambayo yameandaliwa na kituo cha sheria na haki za binadamu nchini LHRC kwa udhamini wa shirika la kimataifa la wanawake la UN-WOMEN,mafunzo ambayo yamefanyika kwa siku mbili Jijini Dra es salaam.
Wakizungumza na wanahabari wakati wakitoa tamko lao juu ya mwenendo wa uchaguzi huo mgombea ubunge wa jimbo la ubungo kwa tiketi ya ACT-wazalendo Mama NYANJURA NYARINDO pamoja na mgombea ubunge wa ubungo kwa tiketi ya chama cha TLP Mama GODLIVA MANUMBA wamesema kuwa katika hatua hii ya kampeni wanawake wamekuwa wakiwekwa nyuma sana na vyombo vya habari pamoja na wadau wa uchaguzi jambo ambalo wamesema linazidi kuwarudisha nyumba katika harakati zao za uchaguzi huo.
Aidha wamesema kuwa changamoto nyingine ambayo inawarudisha nyuma wagombea wanawake katika uchaguzi wa mwaka huu ni changamoto ya rasilimali ambayo imekuwa ikiwafanya kushindwa kuendesha shughuli zao za kampeni huku wakiwaomba wadau kuhakikisha wanawasaidia ili waweze kufanikisha ndoto zao katika uchaguzi huu.

Nao waandaaji wa Mafunzo hayo ambayo ni LHRC kupitia Afisa Program wa dawati la jinsia na watoto NAEMY SILAYO amesema kuwa lengo kuu la kuandaa mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wagombea wanawake wa udiwani na ubunge katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania ili waweze kupambana na kasi ya uchaguzi iliyopo sasa nchini.
Afisa Program wa dawati la jinsia na watoto kutoka kituo cha sheria na haki za Binadamu LHRC ,NAEMY SILAYO akizngumza na wanahabari juu ya mafunzo hayo na malengo yao kwa wagombea hao.
Amesema moja kati ya malengo ya mafunzo hayo pia ni kuhakikisha kuwa wanawatoa wanawake hao katika fikra za kuamini kuwa wanaweke hawawezi na kuwarudisha katika fikra za kuamini kuwa wanawake wanaweza kama wakiwa na nia na kujituma pamoja na kuwapa mbinu mbalimbali ambazo wanaweza kuzitumia katika uchaguzi huo ili waweze kushinda nafasi ambazo wanawania.
Aidha NAEMY amevitaka vyama vya siasa kuhakikisha kuwa vinatoa nafasi sawa kwa wanawake na wanaume katika kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ambapo kwa sasa amekiri kuwa nafasi ya wanawake ndani ya vyama vya siasa bado ni finyu.










No comments: