Na Optatucy stan-Dar es salaam
Mgombea wa urais
kupitia chama cha demokrasia na maendeleo chadema na anayeungwa mkono na vyama
vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi ukawa mh Edward ngoyai lowasa
amewaahidi wakazi wa Dar es saalam kuwa kama watampa ridhaa ya kuongoza nchi
atahakikisha kuwa ndani ya siku mia moja ya utawala wake anapunguza foleni
pamoja na kuhakikisha madawa yanakuwepo ya kutosha kwenye hospitali.
Mh Edward lowasa
ameyasema hayo katika mkutano uliohudhuliwa na mamia kwa maelfu ya wakazi wa
jiji la Dar es saalam kwenye viwanja vya Tanganyika pakers kawe.Mh lowasa
amesema kuwa serikali yake itaweka
misingi ya utawala bora kwa kujenga kituo maalum ambacho kitakuwa kinatumika na
wananchi kuajili ya kupata taarifa mbalimbali toka selikalini.
Akishangliwa na mamia
kwa mami ya watu waliojitokeza katika mkutano huo Mh lowasa amesema jambo kubwa
ambalo linasumbua kichwa chake kwa mda mrefu ni umaskini wa watanzania ambao
umesababishwa na chama kilichopo madarakani.
Mh Lowasa ambae ametumia
muda mwingi kuelezea namna atakavyopambana na umaskini amesema kuwa”UMASIKINI
SIO KIPAJI WALA SIO NEEMA TOKA KWA MUNGU NACHUKIA UMASIKINI AND IAM TIRED OF
IT.Mwisho wa kumnukuu.
Mh lowasa
anayejipambanua kwa utokomezaji wa umasikini amehoji kuwa kama uingereza
wameipa elimu kipaumbele kuliko vitu vyote kwanini isiwe Tanzania? Amehoji.Hata
hivyo mh lowasa ameahidi kuwa pindi selikali yake itakavoingi madarakani suala
la elimu litakuwa mbele kuliko jambo lingine lolote.
Kwa upande wake naibu
katibu mkuu wa chama cha Chadema bara JONH JONH MNYIKA ameionya tume ya taifa ya uchaguzi
kutokufwata maelekezo ambayo yanatolewa na watawala wa Nchi huku akisisitiza
kuwa mwaka huu ni mwaka wa mabadiliko na watanzania wameamua kuyafanya hivyo
daftari la kupiga kura liheshimiwe.
Mnyika amewaomba
watanzania kuwachagua viongozi wa ukawa kwani ndo wenye malengo thabiti ya
kutatua kero zao mbalimbali.
Kwa upande wake mke wa
Edward lowasa mama Regina lowasa amewaomba wakazi wa dare s saalam kutorudi
nyuma maamuzi ambayo tayari wameyafanya wayatekeleze kwa vitendo siku ya kupiga
kura kwa kuchagua viongozi wa ukawa katika ngazi zote za urais,ubunge,na
udiwani.
Mwenyekiti wa chama cha
demokrasia na maendeleo chadema Bw Freeman Mbowe amewambia watanzani kuwa siku
ya terehe 24 mwezi huu ni siku ambayo watanzania hawapaswi kulala ni siku
ambayo wanatakiwa kijianda kikamilifu kuajili ya kufanya maamuzi ambayo
yatakuwa ni maamuzi ya busara kwao na kwa vizazi vijavyo.
No comments:
Post a Comment