Tuesday, October 6, 2015

Swala Tanzania kuanza uchimbaji mafuta Kilombero



Kampuni ya mafuta na gesi ya Swala Tanzania plc  inapenda kutaarifu  kwamba  imechagua eneo kwa ajili ya uchimbaji wa kisima cha mafuta na utafutaji kwa mwaka  2016 ambao utafanyika kwenye eneo tarajiwa la Kito  kwenye leseni ya Kilosa- Kilombero.
 Akifafanua kuhusu kuanza kwa uchimbaji huo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Swala, David Mestres Ridge alisema kuwa tafsiri ya marudio ya 2013 na 2014 ya takwimu za mirindimo zimesababisha  kuboreshwa kwa uelewa wa eneo tarajiwa  la Kito, huku akiongeza kuwa tathmini za mirindimo zilizopo zimebainisha kuwepo umbo la ziada kwenye ufa unaopakana na bonde  hilo la Kito lilopo upande wa magharibi mwa bonde la Kilombero.
“Tafsiri mpya za takwimu kwenye bonde la  Kito  zimeonesha kuongezeka kidogo kwa ukubwa muundo wa ramani iliyotengenezwa awali wakati mapitio ya awali ya muundo huo wa ziada  yameiwezesha kampuni  kukubaliana na hazina  iliyopo kwenye bonde la Kilombero.
 Ridge alisema, “Mapitio ya kiufundi kwa Bonde la Kilombero yanaonesha matarajio ya Kito  yatakuwa makubwa  na yametoa vidokezo vya matumaini vya kuwepo rasilimali muhimu ndani ya bonde hilo. Kampuni ya Swala ipo kwenye mchakato wa kumalizia  tathmini ya athari za mazingira (EIA) kwenye maeneo yaliyoteuliwa kwa ajili ya uchimbaji na pia kutafuta wakandarasi wa uchimbaji kwa ajili ya kisima cha utafutaji mafuta cha Kito kwa mwaka 2016.

Kuhusu Swala:

Swala ni kampuni iliyo chini ya kivuli cha Swala Energy Limited, kampuni ambayo kwa upande wake iko kwenye orodha ya soko la hisa la nchini Australia (ASX) na ikijulikana kwa kifupi kama "SWE". Swala inamiliki mali katika nchi za Afrika Mashariki zinazopitiwa na mfumo wa bonde la ufa na ina ardhi yenye eneo la zaidi ya kilomita za mraba 17,500. Swala inafanya kazi kwa juhudi na ina mpango wa maendeleo ya biashara ili kuendelea kukua hasa katika majimbo ya Afrika Mashariki yenye nishati ya hydrocarbon.



No comments: