Saturday, October 3, 2015

VIDEO--MNYIKA Amjibu Jaji LUBUVA,awataka wapiga kura kulinda kura zao,

Wakati jana Tume ya Taifa ya uchaguzi nchini Tanzania ikitangaza kuwa sio  lazima kwa wanananchi kubaki maeneo ya vituo vya kupiga kura kwa kisingizio cha kulinda kura,nao umoja wa katiba ya wananchi ukawa wameibuka na kuwataka wananchi na wafuasi wao kupuuza kauli hiyo na kuhakikisha kuwa wanasimama umbali uliowekwa kisheria wa mita mia moja ili kuzuia aina yoyote ya hujuma zinazoweza kufanywa na wapinzani wao.EXAUD MSAKA HABARI anasimulia--------

Akitangaza msimamo huo leo Jijini Dar es salaam katibu mkuu wa chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA JOHN MNYIKA amesema kuwa kauli ya mwenyekiti wa tume ya uchaguzi kuwa wapinzani hao wana ajenda yao ya siri  mwenyekiti huyo aleleze wazi ajenda hiyo anayosema  lakini lengo lao ni kuwapa wapiga kura haki ya kusimamia kura zao na kuhakikisha kuwa hakuna aina yoyote ya uchakachuaji unaoweza kufanyika.

Mnyika amesema kuwa kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi wapiga kura wanatakiwa kukaa umbali wa mita mia moja kutoka kituo cha kupigia kura wakifwatilia kwa ukaribu kura zao zikihesabika na ndicho wanachowaelekeza wapiga kura wao na hakuna sheria itakayovunjwa hivyo akawataka wapiga kura na wafuasi wao ambao wanahitaji kulinda kura zao kuhakikisha  kuwa wanakaa umbali huo ili kufwata sheria zilizowekwa na tume ya taifa ya uchaguzi.

“Ni kweli kuwa tuna mawakala wetu ambao watakuwa wanasimamia kura ndani,na tuna waamini sana lakini tunachokisema sisi wananchi ni mawakala wengine ambao wanaweza pia kutusaidia,tuna uzoefu wa chaguzi nyingi,maeneo mengine mawakala wetu wamekuwa wakiichezewa rafu nyingi bila wao kujua na kujikuta washafungwa goli la mkono,ila tunaamini wananchi wakiwa maeneo ya karibu kufwatilia kila kinachoendelea hakuna mtu anayeweza kumchezea rafu wakala wetu wa ndani”Amesema mnyika.

Ameongeza kuwa kufwatilia matokeo kwa ukaribu ni haki ya mpiga kura yoyote Tanzania kwa mujibu wa sheria na hakuna vurugu wala uvunjaji wowote wa sheria ambao unawea kutokea kama tume ilivyoeleza hapo awali.

Aidha katika hatua nyingine JOHN MNYIKA mbaye pia ni mgombea ubunge wa jimbo la kibamba ameitaka tume ya taifa ya uchaguzi kuhakikisha kuwa inagawa nakala ya daftari la kudumu la wapiga kura kwa vyama vya siasa mapema ili walikague na kujiridhisha kwani kuendelea kulichelewesha ni kuendelea kuleta sintofahamu na kufanya wananchi waamini kuwa kuna aina ya uchakachuaji unaofanywa na tume hiyo.

“Tunaitaka tume igawe daftari kwa vyama vya siasa haraka iwezekanavyo na sio kusema tutawapa halafu hawatoi,kuna uwezekano mkubwa wanachelewesha maksudi ili waje walitoe mwishoni ambapo wanajua kabisa likiwa na makosa hakutakuwa na muda wa kuhoji tena kwani siku ya uchaguzi itakuwa imefika”amesema MNYIKA.

KUHUSU KUKAGUA MFUMO WA UHESABUJI KURA
Baada ya jana tume chaguzi kutangaza rasmi kuwa wataalamu wa tahema kutoka vyama vyote wataruhusiwa kwenda kukagua mfumo utakaotumika kuhesabia kura,Mnyika amesema kuwa kusema hivyo haitoshi na badala yake waruhusiwe mara moja kwenda kukagua na kuangalia kama una mapungufu na sio kuja kupewa nafasi hiyo dakika za mwisho jambo ambalo halitakuwa na faida kwani hawatakuwa na muda wa kutosha kufanya marekebisho katika mfumo huo.
KUHUSU WANAHABARI
Wakati tume ya taifa ikitangaza kuwa wakati wa uchaguzi mkuu waandishi wa habari watakaoruhusiwa kushiriki kutoa taarifa za uchaguzi huo ni wale waandishi wenye press card walizopewa na idara ya habari maelezo pekee,Mnyika amesema kauli hiyo inaweza kuzuia upatikanaji wa taarifa hasa zile za vijijini kwani wanahabari wengi kwa sasa hawana hizo Card na wanafanya kazi,hivyo ni lazima tume iliangalie kwa jicho la pili swala hilo.

No comments: