Sunday, November 22, 2015

Baada ya Zomea Zomea ya Bungeni Juzi,Wabunge wa Cuf Watoa kauli yao Leo--Soma Hapa

Mwenyekiti wa wabunge hao wa chama cha wananchi CUF ndugu JUMA HAMAD OMARY akizungumza
 Na Exaud Msaka Habari
Wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania kutoka chama shiriki cha UKAWA chama cha wananchi CUF wamesema kuwa hakuna mgogoro wa kisiasa unaoendelea zanzibar kama inavyoelezwa na baadhi ya wanasiasa kwani uchaguzi wa Zanzibar umekamilika na kinachosubiriwa ni kutangwaza kwa mshindi wa uchaguzi huo ili aweze kuanza kazi mara moja.

Wabunge hao wamesema kuwa hoja ya kuwahadaa watanzania kuwa visiwani huko kuna Mgogoro wa kisiasa ni hoja iliyopandikizwa na chama cha mapinduzi ili waweze kuwaaminisha watanzania kuwa kuna mgogoro jambo ambalo wamesema ni uzushi na kinachoendelea ni ulaghai wa kutaka kupora ushindi alioupata mgombea wa chama hicho ndugu MAALIM SEIF SHARIF HAMAD.
Mbunge wa jimbo la malindi Mh ALLY SALEHE akifafanua jambo
Kaauli hiyo imetolewa na wabunge hao Leo Jijini Dar es salaam katika makao makuu ya chama cha wananchi CUF wakati wakitoa ufafanuzi wa kile kilichotokea Bungeni wakati Rais wa Tanzania akifungua  bunge ambapo wabunge wa vyama vya upinzani wanaojulikana kwa jina La UKAWA waliamua kumpinga wazi aliyekuwa Rais wa Zanzibar Dr shein na kuamua kutoka nje jambo ambalo lilizua taharuki miongoni mwa wabunge ndani ya bunge hilo.

Mwenyekiti wa wabunge hao wa chama cha wananchi CUF ndugu JUMA HAMAD OMARY amesema kuwa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania lipo kwa mujibu wa sheria ambapo bunge hilo linaendeshwa na sheria na kanuni zake na hivyo yanapotokea mambo ya kukiuka kanuni na taratibu za bunge lazima wabunge hao watapaza sauti zao.
Amesema kuwa sheria zinaeleza wazi kuwa anayeruhusiwa kuingia bungeni bila Ruhusa maalum ni Rais wa Tanzania Pekee lakini wengine wanastahili kupata ruhusa ya wabunge wenyewe ambapo amesema kuwa swala la Rais wa Zanzibar kuingia bungeni walishalipinga kw barua kama utaratibu unavyoeleza lakini maombi yao yalizarauliwa na ndipo walipoamua kumpinga wazi wazi mbela ya Dunia.


Amesema kuwa wanachopinga na kupigania ni haki ya wanzanzibar inayotaka kuporwa na watu wachache kwani wanaamini kuwa ili Rais Magufuli awe Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ni lazima MAALIM SEIF SHARIF HAMAD atangazwe kuwa Rais wa Zanzibari kwani kura zilizowachagua ni zile zile.
Amesema kuwa kilichowafanya wabunge wa upinzani kupinga kuingia kwa viongozi wa zinzibar bungeni Juzi ni kutetea katiba ya Zanzibar ambayo inasema  muda wa Rais wa Zanzibar umekwisha malizika na kukosa uhalali wa bunge kuedelea kukiwa hakuna uwakilishi iliokamilika kutoka visiwani humo.


Akizungumza katika mkutano huo na wanahabari mbunge wa jimbo la malindi Mh ALLY SALEHE amesema kuwa katika vuta nikuvute ya Juzi bungeni spika wa bunge Mh JOB NDUGAI alivunja kanuni za bunge kuwa kuruhusu askari wa kawaida zaidi ya 40 ikiwa ni pamoja na mlinzi wa Rais aliyetumika kuleta bahasha yenye jina la waziri mkuu kuingia ndani ya bunge kinyume na sheria jambo ambali amesema lilihitaji maombi maalumu na yaridhiwe na bunge nzima ndipo afanye hivyo.

Wabunge hao wameapa kuhakikisha kuwa wanapigania haki ya wanzanziabari juu ya Rais waliyemchagua ndani na nje ya bunge hadi kuhakikisha kuwa Mgombea wa chama Cha wananchi Cuf anatangazwa kuwa Rais wa zanzibar

No comments: