Tuesday, November 24, 2015

Lowasa Alivyowatembelea wachmbaji waliofukiwa na kifusi,Mafuriko yakatokea tena,tizama hii

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akimsalimia na kumpa pole mmoja wa wachimbaji wadogo walionusurika kufa kwenye machimbo ya Nyangarata yaliyopo wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Joseph Burure Robi (44) alipozulu Hospitali ya Wilaya ya Kahama mkoani humo jana kuwapa pole. Robi alipozinduka hospitalini alihoji iwapo Lowassa ameshinda urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu
Wananchi wa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga wakisukuma gari jana alilokuwa amepanda Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa alipokuwa akitoka Hospitali ya Wilaya ya Kahama kuwapa pole waathirika wa machimbo ya Nyangarata walionusurika kifo ambapo wamelazwa hospitalini hapo

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akiwasalimia wananchi waliofurika katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga alipokwenda kuwapa pole waathirika wa machimbo ya Nyangarata jana



No comments: