Sunday, December 20, 2015

WAZIRI MKUU AWASILI MKOANI LINDI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akipungia mkono wakazi wa mkoa wa Lindi mara baada ya kuwasili mkoani humo ikiwa ndio ziara yake ya kwanza tangia kuteuliwa kwake.

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Habari,Utamaduni ,Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mtama  Mhe.Nape Nnauye mara baada ya kuwasili mkoani Lindi.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Zamani wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe, anayewaangalia katikati ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye wakati wa mapokezi kwenye uwanja wa ndege wa mkoa wa Lindi.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa jeshi mkoani Lindi waliojitokeza kumpokea kwenye viwanja vya ndege mkoani Lindi.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Halmashauri wilaya ya Lindi Vijijini Ndugu Matei B. Makwinya.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

No comments: