Mwanachama wa PPF, Angela Mgulu, akitoa ushuhuda wa Fao la Uzazi , wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.
HOTUBA
YA
MGENI RASMI
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO
MHESHIMIWA DKT. ASHATU KIJAJI (Mb)
WAKATI WA UFUNGUZI
WA
MKUTANO WA 25
WA MWAKA WA WANACHAMA NA WADAU WA
MFUKO WA PENSHENI WA PPFMwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni wa PPF, Ndugu
Ramadhani Khijjah;
Ndugu Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya
Mfuko wa Pensheni wa PPF;
Mwenyekiti na Wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) ;
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya
Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi Irene Isaka;
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni
wa PPF, Ndugu William Erio;
Viongozi wote wa Serikali Kuu,
Serikali za Mitaa na Vyama vya Wafanyakazi mliopo hapa;
Ndugu Wanachama na Wadau wa Mfuko wa
Pensheni wa PPF;
Watoa Mada na Wajadili Mada;
Washiriki wa Mkutano huu;
Wanahabari;
Wafanyakazi wa PPF;
Mabibi na Mabwana.
Awali
ya yote napenda kuchukua fursa hii kukushukuru wewe binafsi Mwenyekiti wa Bodi
ya Wadhamini wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Wajumbe wa Bodi yako na Menejimenti ya
Mfuko wa Pensheni wa PPF kwa heshima mliyonipa ya kunialika kuja kufungua
mkutano wenu huu wa 25 wa mwaka wa Wanachama na Wadau wa PPF.
Nichukue
pia fursa hii kwa niaba ya Serikali ya awamu ya tano kuwashukuru wanachama na
wadau wote kwa kufika na kushiriki kwenye mkutano huu wa 25 wa mwaka wa
wanachama na wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF.
Aidha ningependa kuupongeza
Mfuko wa Pensheni wa PPF kwa kuandaa mkutano huu wa kila mwaka kwa mara ya 25
mfulululizo. Sote tunafahamu kuwa,
mikutano ya namna hii ni muhimu kwa ajili ya ushirikishwaji, ubadilishanaji
mawazo na kupokea maoni kwa nia ya kuboresha utendaji na utoaji huduma kwa
wananchama na jamii kwa ujumla. Utaratibu
huu unaimarisha uwazi na uwajibikaji na kuongeza imani ya wananchi na wanachama
kwa Mifuko yao.
Ndugu
Mwenyekiti wa Bodi, wakati unanikaribisha pamoja na mambo
mengine umeelezea ushiriki wa PPF katika kutekeleza mada kuu na kwa kifupi
umeweza kuelezea mafanikio ambayo Mfuko umeyapata tangu Mkutano uliopita. Umeeleza
jinsi Mfuko wenu ulivyoweza kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu hii ili kuendana
na mabadiliko yanayotokea kwenye jamii pamoja na mafanikio ya Mfuko wa Pensheni
wa PPF tangu mkutano uliopita ambayo ni kuongezeka kwa mapato yanayotokana na
michango na uwekezaji, kukua kwa thamani ya Mfuko wa PPF na kufikia zaidi ya shilingi
trillioni mbili hadi mwishoni mwa Juni 2015. Nawapongeza sana kwa mafanikio
hayo hususani kwenye uwekezaji wenye tija eneo ambalo lina matatizo kwenye
Taasisi nyingi.
Vilevile umeelezea jinsi Mfuko
wenu ulivyojikita katika matumizi ya TEHAMA kwenye utoaji wa huduma; kutanua
wigo wa kuwasomesha watoto wa wanachama wenu wanaofariki wakiwa kwenye ajira; kuendelea
kutoa mikopo ya SACCOS ambapo mpaka sasa mmetoa jumla ya shilingi bilioni 91.34
kwa wanachama wenu, kuanzishwa kwa mfumo mpya wa “Wote Scheme “ kwa sekta
isiyokuwa rasmi, na mafao mapya ya Uzazi. Huu ni ubunifu wa hali ya juu
unavyoonesha jinsi mnavyowajali wanachama wenu.Kwa niaba ya Serikali napenda
kuwapongeza sana kwa mafanikio hayo.
Mambo hayo niliyoyataja
pamoja na Taarifa yako kuwa Mfuko wenu umeshapata tuzo tatu za kimataifa kutoka
Shirikisho la Hifadhi ya Jamii duniani (ISSA) na tuzo mbili za hesabu bora
kwa miaka miwili mfululizo kutoka Bodi
ya Wahasibu na Wakaguzi wa ndani (NBAA), na kuwa sasa huduma
zenu ni za kiwango cha kimataifa kama inavyodhihirishwa na cheti utoaji huduma bora cha kimataifa ( ISO
9001: 2008 Certified) yamenifurahisha sana.
Kwa
niaba ya Wizara ya Fedha napenda kuwaarifu
kuwa Serikali ina imani na utendaji
mzuri wa Mfuko wenu na naipongeza sana Bodi, Menejimenti na Wafanyakazi wa PPF
kwa hilo
Ni wazi kuwa wadau mlioko hapa na wengine
watakaopata Taarifa hizi kupitia kwenye vyombo vya habari watachangamkia fursa
ya kujiunga na Mfuko wa PPF ili waweze
kunufaika na huduma za kisasa na mafao bora yanayotolewa na Mfuko wenu.
Ndugu
Mwenyekiti wa Bodi, nimalizie kwa kuzungumzia baadhi ya
changamoto ulizozitaja kama ifuatavyo:
(i)
Kuhusu waaajiri wasioleta michango kwa
wakati ninaagiza kwamba waajiri wa namna hiyo waache tabia hiyo mara moja kwani
ni uvunjaji wa sheria na unaleta usumbufu usio wa lazima kwa wastaafu na Mifuko.
Serikali imeshatoa agizo la kuwataka waajiri wote kuhahakisha wana mikataba na
wafanyakazi wao na wanawaandikisha katika Mifuko ya hifadhi ya jamii na
kuwachangia kama sheria inavyotaka. Ninaagiza kwamba hatua za kisheria zichukuliwe
kwa kuwashtaki waajiri wote wanaochelewesha michango na kuziomba mahakama kesi
hizo ziamuliwe kwa haraka ili kuondoa kero kwa wananchi na Mifuko.Waajiri wakichangia
kwa mujibu wa sheria watawawezesha wanachama kupata mafao yao kikamilifu na kwa
wakati; wakati huo huo kuifanya mifuko kubuni mafao zaidi kwa wanachama badala
ya kutumia muda mrefu kufuatilia kesi za michango mahakamani.
(ii)
Kuhusu
madeni ya Serikali kwa PPF,tayari suala
hili linashughulikiwa ambapo tayari Wizara imeshaiagiza Benki Kuu kuandaa non-cash bond ambayo itatolewa kwa Mfuko ikiwa ni mkakati wa
kulipa madeni hayo.Pia Serikali imeshaanza na itaendelea kuhakikisha michango
ya pensheni kwa wafanyakazi wa taasisi zinazopata ruzuku kutoka Serikalini
inalipwa kwa wakati.
(iii)
Kuhusu suala la mafao ya kujitoa, Wizara
yangu itawasiliana na Wizara ya Sera,
Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu ili kupata ufumbuzi wa kudumu wa suala
hili kwani ni dhahiri kuwa linakwenda kinyume cha kanuni za hifadhi ya jamii
duniani na halina tija kwa wafanyakazi na Mifuko.
Naomba
kabla sijamaliza nami niwape changamoto zifuatazo:
i)
Mfuko uendelee kuboresha huduma kwa wanachama
wake kwa kuzingatia mahitaji ya sasa ili kuwavuta watu wengi zaidi kujiunga na
PPF
ii)
Kwa kuzingatia mada kuu ya mkutano, Mfuko uangalie
uwekezaji katika maeneo ambayo bado haujaingia kwa kuzingatia kanuni za
uwekezaji zilizotolewa na Benki Kuu ya Tanzania kwa kushirikiana na SSRA baada
ya kujidhihirisha kuwa uwekezaji huo utakuwa na tija ili kujiongezea mapato na
hivyo kuwa na uwezo mzuri zaidi wa kuboresha mafao kwa wanachama wake.
Baada ya kusema maneno hayo,
naomba sasa kutamka kwamba mkutano huu wa 25 wa mwaka wa wanachama na wadau wa
PPF umefunguliwa rasmi.
Asanteni sana kwa kunisikiliza.
|
No comments:
Post a Comment