Tuesday, March 29, 2016

MSANII KLEYAH AWAPAGAWISHA MASHABIKI VIWANJA VYA ESCAPE ONE MKESHA WA PASAKA


Msanii wa usic wa kizazi kipya nchini Tanzania anayekuja kwa kasi kwa sasa KLEYAH mwishoni mwa wiki hii aliwapagawisha mashabiki wake wa Jiji la Dar es salaam katika viwanja vya ESCAPE ONE kwa kutoa burudani kali ya kutambulisha wimbo wake mpya wa AFRICAN DRUM ambao unamuweka juu kwa sasa katika anga za music wa kitanzania. 


 Katika tamasha hilo ambalo liliandaliwa na Clouds FM lililowakutanisha wasanii maarufu nchini akiwemo Dogo Janja,Godzila,Q CHIEF,MB DOG na wengine wengi Msanii KLEYAH Alipata nafasi ya kutambulisha nyimbo yake mpya na kupokelewa kwa sangwe kubwa kutoka kwa watanzania waliohudhuria Tamasha hilo lililofanyika Usiku wa mkesha wa pasaka.
 Akizngumza baada ya kufanya shoo yake msanii huyo aliwashukuru watanzania kwa ushirikiano na mapokezi makubwa aliyoyapata na kuahidi kuendelea kutoa burudani na kuhakikiaha kuwa anawsaburudisha watanzania kwa kupitia kipaji chake.
Hapa kuna picha zote za tukio hilo unaweza kuzitazama















No comments: