Sunday, May 1, 2016

FUKUTO LA MGOGORO NDANI YA CHAMA CHA ADC,BAADHI YA VIONGOZI WAMJIA JUU MSAJILI WA VYAMA KWA KUCHOCHEA MGOGORO HUO

Naibu katibu mkuu wa chama cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE ADC Ndugu DOYO HASSAN DOYO akionyesha baadhi ya nyaraka mbalimbali ambazo zinaonyesha jinsi msajili wa Vyama vya siasa alivyokiuka katiba ya chama hicho katika maelekezo yake ya kutaka mwenyekiti wa chama hicho arejeshwe madarakani baada ya kutimuliwa na Bodi ya wadhamini ya chama hicho
 Mgogoro wa kisiasa ulioibuka ndani ya chama cha upinzani nchini Tanzania cha Aliance for democratic change ADC baina ya mwenyekiti wa chama hicho SAID MIRAAJ ABDULLA na bodi ya wadhamini ya chama hicho mgogoro ambao umesababisha hadi mwenyekiti huyo kusimamishwa ndani ya chama hicho  umeendelea kuchukua sura mpya baada ya viongozi wa chama hicho kuibuka leo na kumkaanga msajili wa vyama vya siasa nchini jaji FRANSIS MUTUNGI—anandika Exaud Mtei kutoka Dar es salaam---

Ikiwa ni miezi sita sasa tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu nchini Tanzania ambao ulimalizika kwa chama hicho kushindwa kufurukuta kikamilifu katika uchaguzi huo kuliibuka sintofahamu juu ya maswala ya kisiasa ndani ya chama hicho huku mwenyekiti akituhumiwa kutumia nafasi yake vibaya kuivuruga katiba ya chama hicho ikiwa ni pamoja na kuwafukuza baadhi ya viongozi.
Baada ya mgogoro huo kuonekana kukua kwa kasi hatimaye ulimfikia msajili wa vyama vya siasa nchini ambaye kwa upande mwingine ndiye mlezi wa vyama vya siasa nchini Tanzania ambapo aliamua kuchukua hatua mbalimbali ambazo zinaonekana kupingwa na uongozi uliosalia ndani ya chama hicho chenye makao makuu yake Buguruni Jijini Dar es salaam.


Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam Naibu katibu mkuu wa chama hicho Doyo Hassan Doyo ameeleza kuwa mnamo tarehe 27 mwezi wanne mwaka 2016 walipokea barua kutoka kwa msajili wa vya vya siasa nchini inayoiagiza bodi ya wadhamini kuwa uongozi uliochanguliwa kihalali urejeshewe mamlaka yake badala ya bodi ya wadhamini kuchukua mamlaka ya uendeshaji wa shughuli za chama kuwa si halali,barua ambayo wamedai inamapungufu makubwa na hawakubaliani na agizo hilo.

“Baada ya kupokea barua hiyo tuligundua kuwa kuna mapungufu makubwa sana,kwanza haikuzingatia matakwa ya katiba ya chama chetu zaidi ya kubeba ushabiki wa msajili na ishara ya wazi kutaka kuuendeleza mgogoro huo ambao ulishapatiwa ufumbuzi kwa mujibiu wa katiba ya chama,pia ilijaa upotoshaji mkubwa wa Tafsiri ya katiba yetu ya ADC,lakini pia haina hoja zenye msingi ya kuonyesha dhamira nzuri za kumaliza mgogoro huo” Ameeleza naibu katibu mkuu huyo ambaye naye alikuwa ametimuliwa hapo awali na mwenyekiti wa chama hicho.

Amesema kuwa kitendo cha msajili kutetea uongozi huo wa mwenyekiti kuendelea kuwepo madarakani inaonyesha wazi kuwa msajili huyo ana maslahi na uongozi huo hivyo wamemtaka kuacha mara moja kwani mwenyekiti wa chama hicho amesimamishwa kwa mujibu wa katiba halali ya chama hicho.
Wanahabari kazini
CHANZO CHA MGOGORO CHATAJWA
Imekuwa ikielezwa kuwa kumekuwa na mambo kadhaa ambayo yamesababisha mgogoro huo ndani ya ADC huku uchaguzi wa marudio visiwani Zanziabar ukitajwa kama moja ya sababu kubwa ya kuchochea mgogoro huo ambapo ilisemekana kuwa mwenyekiti wa chama hicho alipingana wazi wazi na  ushiriki kwa chama chao katika uchaguzi wa marudio visiwani Zanzibar ambao mgombea wa chama hicho HAMAD RASHID alishiriki na kuambulia asilimia tatu ya kura zote.

Sababu nyingine iliyokuwa ikitajwa na baaadhi ya wachambuzi wa maswala ya kisiasa ni ile ya mwenyekiti huyo kutumia kiti chake kuwasimamisha uanachama baadhi ya wanachama wao akiwemo mkurugenzi wa ulinzi na usalama wa chama hicho ambapo ndicho kilisababisha kuongozeka kwa mgogoro huo.

Akieleza sababu za mgogoro huo huku akikanusha sababu zote zilizokuwa zinatajwa Naibu katibu mkuu huyo amesema kuwa sababu kubwa ya kumsimamisha mwenyekiti wa chama hicho ni hatua yake ya kuzungumza maswala ya chama hicho mbele ya wanahabari hasa mambo ambayo hayana Baraka ya chama hicho na mbaya Zaidi kuzungumza maswala ya kukitisha na kukivuruga chama hicho.

“Mwenyekiti wetu alifika mahali anamua kukivuruga chama hasa pale alipotangaza kwa wanahabari kuwa Tarehe 11 atakifumua na kuweka mambo ya chama wazi,sisi kama viongozi wa taasisi yenye taratibu,katiba na miongozo yake hatuwezi kusubiri kuona mtu kama huyo akikivuruga chama na ndio sababu iliyotufanya kumsimamisha mwenyekiti huyu.ameeleza Doyo

Ameendelea kusema kuwa sababu nyingine ambazo zimekuwa zikitajwa kusababisha mgogoro huo ni uzushi na uongo kwani kutofautiana mitizamo kuhusu uchaguzi wa Zanzibar hakuwezi kuleta mgogoro kwani hayo ni maswala ya kawaida katika siasa.

Mwenyekiti wa chama hicho SAID MIRAAJ ambaye amesimamishwa na bodi ya wadhamini ya chama hicho 
TAHADHARI KWA MWENYEKITI HUYO
Aidha katika hatua nyingine chama hicho cha ADC kimemtaka mwenyekiti huyo kaucha kufanya mikutano na wanahabari vichochoroni nje ya ofisi na badala yake kama anajiamini kuwa ni mwenyekiti wa chama hicho halali ajitokeze na azungumze ndani ya ofisi zake kwani kuendelea kuzungumza nje ya chama ni kuonyesha ni jinsi gani anavyoichezea katiba ya chama hicho.

“Tunashangaa tunaona tu kwenue vyombo nya habari akizungumza maswala ya chama ila hatujui anazngumzia wapi,mwenyekiti gani anafanya mikutano yake na wanahabari nje ya ofisi yake,kama ni mwenyekiti halali aje azungumze ndani ya ofisi za chama hapa”Ameeleza Naibu katibu mkuu huyo.

Mwisho kabisa Naibu katibu mkuu huyo amelitaka baraza la vyama vya siasa nchini kuacha utapeli wa kisiasa kuwabeba viongozi ambao wana matatizo na vyama vyao ili kuepusha migogoro isiendelee katika vyama vyao huku akiwataka wanachama na wapenzi wa chama hicho kutulia na kuendelea kuwa na Imani na chama chao hasa kipindi hiki cha mgogoro huu.

No comments: