Tuesday, May 3, 2016

MAMIA WAJITOKEZA KUMUAGA 'KAMANDA' GABRIEL MWAIBALE

 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Gabriel Peter Mwaibale aliyefariki juzi nyumbani kwao Mabibo jijini Dar es Salaam ambapo mazishi yake yatafanyika leo Kijiji cha Mpuga Wilayani Rungwe mkoani Mbeya.
 Baba mgogo wa marehemu Kulwa Mwaibale (kulia), akitoa maelekezo kwa waombolezaji kabla ya kuanza safari ya kuusafisha mwili huo hadi Tukuyu Rungwe mkoani Mbeya kwa mazishi.
 Babu wa marehemu Mchungaji Ambakisye Mwaibale akitoa heshima za mwisho.
 Rafiki zake marehemu Gabriel wakiwa katika msiba huo.
 Michango mbalimbali ikipokelewa.
 Wakina mama wakiwa katika msiba huo.
 Dada zake Gabriel wakilia katika msiba huo.
 Shangazi wa marehemu Gabriel, Ambwene Anyitike (kulia), akitoa heshima za mwisho wakati wa kuuaga mwili huo.
 Mtoto wa kaka yake Gabriel, Helena Mathias (katikati), akilia kwa uchungu kwa kupotelewa na baba yake mdogo ambaye alikuwa ni kipenzi chake mkubwa.
 Uagaji ukiendelea.
 Rafiki zake Gabriel wakitoa heshima zao.
 Kaka wa marehemu akitoa heshima za mwisho.
 Ndugu jamaa na marafiki wakiwa kwenye msiba huo.
 Dada ya marehemu Elines Mwaibale (kushoto), akiwa na bibi wa marehemu wakati wa kuaga mwili huo.
 Shughuli ya uagaji ikiendelea.
 Dada wa marehemu Neema akiwa ameanguka chini baada ya kupoteza fahamu wakati wa kuaga mwili huo.
 Baba mdogo wa marehemu Kulwa Mwaibale na jirani yake na marehemu wakiweka vizuri mfuni wa jeneza baada ya shughuli ya kuaga mwili huo kukamilika.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Gabriel tayari kwa safari ya kwenda mkoani Mbeya kwa mazishi yaliyofanyika leo kijiji cha Mpuga Lutengano Tukuyu mkoani Mbeya.
Gari likiwa tayari kwa safari hiyo. 

No comments: