Tuesday, May 31, 2016

NAPE AMJULIA HALI BABA WA DIWANI WA CHADEMA

 Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akisalimiana na  Diwani wa kata ya Mtama Bw. Hassan Omary Nyimbile (CHASEMA) mara baada ya kuwasili kwenye hospitali ya Nyangao kumjulia hali Baba wa Diwani huyo aliyelazwa hapo. .
 Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akipewa maelezo juu maendeleo ya hali ya Mzee Omary Nyimbile, baba wa Diwani wa kata ya Mtama Bw. Hassan Omary Nyimbile (CHADEMA) aliyelazwa katika Hospitali ya Nyangao.
Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akimuangalia Mzee Omary Nyimbile, baba wa Diwani wa kata ya Mtama Bw. Hassan Omary Nyimbile aliyelazwa katika hospitali ya Nyangao.
 ………………………………………………………………………………………

Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye amemjulia hali Mzee Omary Nyimbile, baba wa Diwani wa kata ya Mtama Bw. Hassan Omary Nyimbile .
Mhe. Nape ambaye yupo kwenye ziara ya utekelezaji wa ahadi zake jimboni kwake na kuonana na wananchi alifika kwenye hospitali ya Nyangao mwishoni mwa wiki iliyopita na kupokelewa na Diwani huyo wa kata ya Mtama kupitia Chama Cha Chadema.
Mheshimiwa Mbunge wa Mtama alimjulia hali Mzee Omary na kumtakia heri ya kupona haraka.
Kitendo cha Mhe. Mbunge kumjulia hali baba wa Diwani wa Chadema kimewashangaza wengi ambao walidhani viongozi hawa hawatoweza kuzungumza kutoka na hali ilivyokuwa wakati wa uchaguzi.

No comments: