Sheikh JALALA akifungua Rasmi maktaba ya vitabu vya mafunzidho mbalimbali ya kidini Iliyopo jijini Dar es salaam yenye lengo la kuwasaidia waumini wa Dini mbalimbali katika kupata mafunzo ya dini zao |
Vijana nchini Tanzania
wametakiwa kujijengea utaratibu wa kujisomea vitabu mbalimbali vya dini ili
waweze kujua ni jinsi gani watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini waliishi
kwa Amani na njia za kuweka maelewano katika jamii.
Wito huo umetolewa Jijini Dar es salaam na Shekh Mkuu wa madhehebu ya SHIA nchini Tanzania Sheikh
HEMED JALALA wakati akifungua rasmi maktaba mpya iliyopo Jijini Dar es salaam
yenye vitabu ya mafubdisho mbalimbali ya dini zote.
Amesema kuwa makatba
hiyo imekuja kwa ajili ya kuwasaidia vijana na watanzania mbalimbali bila
kujali Itikadi zao za kidini katika kupata mafundisho mbalimbali
yatakayowasaidia kuwatoa katika matatizo mengi yanayowakabili katika jamii.
Ameongeza kuwa vijana
wa Tanzania ndio nguvu kazi ya taifa hivyo maktaba hiyo imekuja kwa ajili ya
kuwaelekeza ni jinsi gani wanaweza kuwa tegemeo katika taifa la Tanzania na
kuachana na changamoto mbalimbali zinazowakabili zikiwemo za utumiaji wa
madawa ya kulevya ambazo zimezidi kukithiri katika taifa kwa sasa.
Sheikh JALALA ameeleza
kuwa kijana yoyote anayehitaji kuwa na uelewa mkubwa wa maswala ya Amani na
dini ni lazima aitafute elimu katika vitabu mbalimbali vilivyoandikwa na
viongozi wakubwa jambo ambalo ameeleza kuwa maktaba hiyo imekuja mahususi kwa
ajili ya kuwasaidia watanzania kuleta maelewano,Amani,na masikilizano kwa jamii yote.
Ufunguzi wa maktaba
hiyo Jijini Dar es salaam umekwenda sambamba na maadhimisho ya kumbukumbu ya
kuzaliwa kwa imam na kiongozi wa 12 baada ta mtume ambaye alikuwa katika mstari
wa mbele katika kuahamasisha umoja,maelewano,masikilizano duniani ambapo
ameongeza kuwa maktaba hiyo pia itatumika kuwapa nafasi watu kusoma mafunzo
mbalimbali ya kiongozi huyo.
No comments:
Post a Comment