Friday, May 6, 2016

SHIRIKA LA WATED NCHINI LAWAKUTANISHA WANAFUNZI WA KIKE DAR KUJADILI HAKI ZAO,SWALA LA SHERIA YA NDOA NA MKANGANYIKO WAKE LAIBULIWA

Catherine Tundaraza Moja kati ya wanafunzi walioshiriki katika Warsha hiyo akichangia maswala mbalimbali yaliyokuwa yakijadiliwa na wataalamu hao leo
Na Exaud Mtei Dar es salaam-0712098645

Wakati dunia na Tanzania kwa ujumla ikiwa katika harakati za kumkomboa mtoto wa kike hususani katika haki zake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa sera ya 50/50 inafikiwa,bado Tanzania imetajwa kuwa na chanamoto nyingi zinazomgusa mtoto wa kike huku serikali ikitakiwa kutekeleza kwa vitendo swala la kumpatia mtoto wa kike haki sawa.
Moja kati ya mambo ambayo yanatizamwa kama changamoto kubwa kwa sasa ni swala la ndoa na sheria ya ndoa nchini ambayo imekuwa katika mikanganyiko mikubwa baina ya wadau wa maswala ya haki za binadamu ambapo sheria hiyo imekuwa ikiruhusu mtoto wa miaka 14 kuolewa huku sheria ya mtoto nchini ikielekeza kuwa mtoto chini ya miaka 18 haruhusiwi kuolewa jambo ambalo limekuwa likipigiwa kelele na wadau mbalimbali wakitaka mabadiliko ya haraka ya sheria hiyo.

Kutokana na maswala mbalimbali yanayowakumbva watoto wa kike nchini hususani wanafunzi na wale waishio vijijini kukosa elimu mahususi kuhusu maswala hayo wadau mbalimbali yakiwemo mashirika ya umma na binafsi yamekuwa yakijitolea kufanya makongamano mbalimbali kuwakutanisha watoto wa kike na kuweza kuzungumza nao na kuwapa elimu juu ya haki na wajibu wa mwanamke katika jamii.


Shirika la WOMEN ACTION TOWARDS ECONOMIC DEVELOPMENT (WATED) wameendesha warsha ya siku moja kwa kuwakutanisha wanafunzi wa shule mbalimbali Jijini Dar es salaam hususani watoto wa kike lengo likiwa ni kuinua uelewa wa wanafunzi hao juu ya haki zao kama watoto wa kike na jinsi gani ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakumba katika mazingira yao.
Katibu wa WATED Tanzania MARIA MATUI akiangumza na wanahabari nje ya warsha hiyo Lep Jijini Dar es salaam
MARIA MATUI ni katibu wa WATED nchini Tanzania ameueleza mtandao huu kuwa lengo kubwa la kuwakutanisha wasichana na wanafunzi wa shule za Dar es salaam ni malengo makuu ya shirika lao kuhakikisha kuwa wanamwelimisha mtoto wa kike na ndicho wanachokifanya kila siku katika shirika lao.


“Leo tumewakutanisha wanafunzi mbalimbali wa shule za secondary Jijini dar es salaam ambapo watakutana na wataalam na wanataaluma wa kada mbalimbali wakiwemo wa maswala ya sayansi na Technologia,wataalamu wa sheria na watu wa ustawi wa jamii lengo ni kuzungumza na watoto wa kike ambao ndio Taifa linalotegemewa waweze kujitambua na kutambua haki zao pamoja na kufahamu nini cha kufanya katika masomo yao ili waweze kufanikiwa”Amesema MARIA MATUI.
Ameongeza kuwa lengo kubwa la kufanya warsha hizo hasa kwa mtoto wa kike na sio wa kiume ni ukweli kwamba katika jamii zetu pamoja na kwamba changamoto za kimaisha ni za wote lakini ni ukweli usiopingika kuwa mtoto wa kike amekuwa akikumbana na changamaoto nyingi Zaidi hivyo wameona waanze na kundi hilo.
Mtandao huu umezumza na baadhi ya wanafunzi ambao walifanikiwa kushiriki katika warsha hiyo ambapo CATHERINE TUNDARAZA na  FLORA JOSEPH wa shule ya kisutu Jijini Dar es salaam wameeleza furaha yao baada ya kupatiwa elimu hiyo muhimu kwa mtoto wa kike wa sasa huku wakiwasihi wahusika kuhakikisha kuwa wanawafikia watoto wengi Zaidi hususani wa vijijini kwani ndio wamekuwa wakikumbana na changamoto nyingi Zaidi kulingana na mazingira wanayoishi. 









No comments: