Monday, May 9, 2016

TAMASHA LA PILI LA MAVAZI YA STARA KUZINDULIWA


TAMASHA la pili la Stara, Stara fashion Week 2016 linatazamiwa kuchukua nafasi yake tena mwaka huu katika ukumbi wa City Garden Restaurant Kamata, June 1 hadi 5.

Tamasha hilo ambalo litafunguliwa na Exhibition ya bure, linakaribisha watu mbalimbali wanawake wanaume na watoto kwa manunuzi ya vitu mbalimbali, kama vile Mabaibui,Mitandio Madera kwa ajila ya Mwezi mtufu wa Ramadhani, evening dresses, kanzu, Udi Hena na vitu vingine pia kutakuwa na wachora heena kwa bei nafuu.




Exhibition hiyo ambayo itakuwa inaanza tarehe 1 June asubuhi ya saa nne hadi saa 12 jioni, itafungwa na maonyesho ya mavazi ya stara kwa wanawake pekee siku ya Jumapili ya tarehe 5 kuanzia saa nne hadi saa 11 jioni.
Katika kilele cha maonyesho hayo kazi za mikono ya wabunifu wa hapa nyumbani wanaobuni mavazi ya stara zitaonyeshwa pamoja na warsha itakayojadili mada mbalimbali ambazo ni pamoja na

1. Jinsi ya kumpata mwenza na kudumisha ndoa
2. Matumizi na Mipango ya Fedha
3. Ujasiriamali Na nyinginezo
Kongamano hilo la wanawake, litakuwa na kiingilio cha shilling elfu 35 VIP na Elfu 50 viti maalum Kwa kujumuisha chakula cha mchana kwa wote na zawadi mbalimbali zitatolewa.

Stara fashion week imedhaminiwa na  Maximalipo, Hijab Couture, Hijabi Central Tz, Kanzu Point, Cordoba School, Speedy Print, I-view Studio, Vayle Springs, AA Shekhozah co. Ltd, City Garden Restaurant, Event Lights, Sofia Production,  Clouds Media na wengineo.

No comments: