Wednesday, June 29, 2016

KIKOSI CHA TWIGA STARS KIPYA CHATANGAZWA-MAJINA HAYA HAPA


Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Mpira wa Miguu ya Wanawake Tanzania, Nasra Juma ametangaza majina ya wachezaji 23 watakaounda kikosi cha Twiga Stars.

Kikosi hicho kinatarajiwa kwenda Kigali, Rwanda Julai 15, 2016 kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Rwanda ikiwa ni mwaliko maalumu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Rwanda (Ferwafa).

Wakati Ferwafa likiingiza mchezo huo wa Julai 17, 2016 kwenye orodha ya michezo inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira na Miguu la Kimataifa (Fifa), lakini Mheshimiwa Rais wa Rwanda Paul Kagame kuwa sehemu ya burudani ya burudani mbele ya wageni wake ambao ni wakuu mbalimbali wanaounda Umoja wa Nchi za Afrika (AU) ambao watakuwa na mkutano wao nchini Rwanda.

Mbali ya soka kama burudani, pia Rais Kagame atatumia mchezo huo kama hamasa kwa wakuu wa nchi ili kutoa kipaumbele kwenye soka la wanawake ambako kwa sasa ni ajira ambayo inakwenda sambamba na kuitikia wito wa kupambana na changamoto za malengo ya millennia (MCC) ambayo pia yanataka wanawake wapate nafasi.


Makipa:
  1. Fatma Omary
  2. Belina Julius
  3. Najiat Abbas

Walinzi:
  1. Stumai Abdallah
  2. Fatma Issa
  3. Anastazia Antony
  4. Happuness Henziron
  5. Maimuna Khamis

Viungo:
  1. Donisia Daniel
  2. Amina Ali
  3. Amina Ramadhani
  4. Fatuma Bashiri
  5. Wema Richard
  6. Fadhila Hamadi
  7. Mwajuma Abdallah
  8. Anna Hebron
  9. Sophia Mwasikili

Washambuaji:
  1. Tumaini Michael
  2. Johari Shaaban
  3. Fatma Idd
  4. Shelder Bonifdace Mafuru
  5. Asha Saada Rashid
  6. Mwanakhamisi Omar


…………………………………………………………………….
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA


No comments: