Friday, June 3, 2016

VIDEO-ACT WAZALENDO WATANGAZA SIKU RASMI YA MAPOKEZI YA KIONGOZI WAO ZITTO NA WALE WA UKAWA

Katibu wa Itikadi mawasiliano na uenezi wa chama cha ACT WAZALENDO Ndugu ADO SHAIBU akizngumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam kuhusu mapokezi ya kumpokea kiongozi yao na mbunge pekee wa chama hicho ZITTO KABWE ambaye naye amekumbwa na timua timua ya bungeni,mapokezi ambayo yatafanyika Jijini Dar es salaam siku ya Jumapili

Na EXAUD MTEI

Story ambayo bado ipo maskioni mwa watanzania walio wengi ni mwenendo wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania na mizengwe yake ambayo imesababisha wabunge saba wa vyama vya upinzani kusimamiswa kushiriki shughuli za bunge kwa vipindi Tofauti tofauti akiwemo mbunge kutoka ndani ya chama cha Act wazalendo Mh ZITTO ZUBERI KABWE na wabunge wa vyama vya UKAWA.

Sakata hilo limeendelea kuchukua Headline katika maeneo mbalimbali ambapo asubuhi hii chama cha ACT wazalendo kupitia kwa kiongozi wao ADO SHAIBU wamejitokeza mbele ya wanahabari kueleza msimamo wa chama chao kuhusu sakata hilo.

Akizungumza na wanahabari leo Katibu huyo wa itikadi mawasiliano na uenezi wa ACT ADO SHAIBU ameeleza kuwa chama hicho kimeandaa mapokezi ya kiongozi wao ambaye amekumbwa na adhabu hiyo mapokezi ambayo yanataraji kufanyika Jijini Dar es salaam na baadae kufwatiwa na mkutano mkubwa wa hadhara ambao umepangwa kufanyika katika viwanja vya ZAKIEM mbagala lengo likiwa ni kuwapa nafasi wabunge hao kueleza ukweli wa yale yanayoendelea bungeni Dodoma.

Pamoja na mandalizi hayo chama hicho kimewaandikia barua makatibu wa vyama vya upinzani ambao nao wanapinga adhabu hiyo kutoka CHADEMA,CUF,na NCCR-MAGEUZI kuwaomba kuungana nao katika mapokezi hayo ambayo yamepewa jina la OPERATION LINDA DEMOCRASIA na bado hawajapata majibu yao lakini wanaamini wataungana nao katika Operation iyo ambayo itafwatiwa na mikoa mingine takribani minne.

Habari24 tv imekuwekea video ya mkutano huo wa wanahabari leo asubuhi

No comments: