Wednesday, September 21, 2016

Kampuni ya Tigo yakabidhi madawati 435 mkoani Tanga leo


Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Goodluck Charles akiongea na wanahabari na wanafunzi ya shule ya msingi Mabawa leo, kwenye hafla ya kukabidhi madawati. Kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Tanga, Thobias Mwilapwa, Katibu tawala wilaya ya Tanga Bi. Faidha Salim na kushoto ni Meneja wa Tigo mkoani Tanga, Patricia Sempinge
Katibu tawala wilaya ya Tanga Bi. Faidha Salim akiongea na wanahabari na wanafunzi ya shule ya msingi Mabawa leo, kwenye hafla ya kukabidhi madawati. Kulia kwake ni mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapwa, Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Goodluck Charles na Meneja wa Tigo mkoani Tanga Patricia Sempinge. Na kushoto kwake mwalimu mkuu Zuwena Msembo.
Mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapwa (kulia)akipokea  dawati toka kwa mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Goodluck Charles(kushoto). Katikati ni mwalimu mkuu wa shule ya mabawa, Zuwena Msembo, Jumla ya madawati 435 yenye thamani ya shilingi milioni 72  yalitolewa na kampuni ya Tigo mkoani Tanga kwenye hafla iliyofanyika shule ya msingi Mabawa leo.
Mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapwa (kulia) akiwa ameketi na mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani(mwenye miwani) na wanafunzi  Amir Kibwana na Pili Ali(kushoto) wa shule ya msingi Mabawa, mara baada ya kampuni ya Tigo kukabidhiwa  435 yenye thamani ya shilingi milioni 72 kwa mkoa wa Tanga leo.
Wanafunzi wa shule ya msingi Mabawa mkoani Tanga wakiwa wameketi kwenye madawati .waliyokabidhiwa na kampuni ya Tigo leo

No comments: