Friday, September 23, 2016

Tigo yatoa simu 800 zenye thamani ya 120m kusaidia zoezi la kusajili watoto chini ya umri wa miaka mitano katika mikoa ya Njomba na Iringa.


Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Nyanda za juu Kusini Jackson Kiswaga akipeana mkono na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Dr Rehema Nchimbi mara baada ya kutoa hotuba wakati wa uzinduzi wa uzinduzi wa awamu ya tatu ya zoezi la usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa, uzinduzi huo ulifanyika jana mjini Iringa.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dr Harrison Mwakyembe akionesha mojawapo ya simu 800 zilizotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo ili kufanikisha zoezi la usajili na utoaji wa vyeti kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano, uzinduzi wa zoezi hilo kwa awamu ya tatu ulifanyika jana mjini Iringa. Kulia kwake ni Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dr Harrison Mwakyembe akikabidhi cheti cha kuzaliwa kwa motto Christina Muyinga, mara baada ya kuzindua uandikishaji na utoaji wav yeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano. Uzinduzi wa awamu ya tatu ya zoezi hilo umefanyika jana mjini Iringa, zoezi hilo limedhaminiwa na Kampuni ya Simuza mkononi ya Tigo ambayo imeipatipatia serikali simu 800 ili kufanikisha zoezi hilo linalofanywa kwa pamoja na RITA, Unicef, VSO na SIDA.
 Baadhi ya wakazi wa Iringa wakiwa katika foleni ya kusubiri kujiandikisha ili kupata vyeti vya kuzaliwa kwa ajili ya watoto wenye umri chini ya miaka mitano, uzinduzi wa awamu ya tatu ya zoezi hilo umefanyika jana mjini Iringa, zoezi hilo limedhaminiwa na Kampuni ya Simuza mkononi ya Tigo ambayo imeipatipatia serikali simu 800 ili kufanikisha zoezi hilo linalofanywa kwa pamoja na RITA, Unicef, VSO na SIDA.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dr Harrison Mwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa mkoa wa Iringa na viongozi wa  tigo  katika makabidhiano ya simu 800 zilizotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo ili kufanikisha zoezi la usajili na utoaji wa vyeti kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano, uzinduzi wa zoezi hilo kwa awamu ya tatu ulifanyika jana mjini Iringa. 

No comments: