Friday, September 23, 2016

TSN YADHAMINI MECHI YA BONGO MOVIE NA BONGO FLAVA KUCHANGIA WAATHIRIKA WA TETEMEKO LA ARDHI BUKOBA


Mkuu wa kitengo cha Masoko na Biashara TSN, Jahu Mohammed Kessy akiwakabidhi wasanii jezi kwa ajili ya mechi ya kuchangia maafaa ya tetemeko la ardhi Bukoba
Kampuni ya TSN  Kwa kushirikiana na Wasanii wa bongo fleva na bongo Movie wamejitokeza kuwezesha mechi maalum kuchangia wahanga wa Tetemeko la Ardhi lililotokea Bukoba mkoani Kagera.

Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Biashara Jahu Mohamed Kessy, amesema TSN imejitokeza kudhamini mechi hiyo itayofanyika uwanja wa taifa, jumaapili tarehe 25 september, na hivyo kuwataka wananchi, mashirika na kampuni mengine binafsi kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kuchangia na kuwezesha misaada kwa wananchi wa Kagera waliopata maafa kutokana na tetemeko hilo la ardhi.


Alisema wao kama TSN wameguswa na janga hili na hivyo mbali na michango yao mingine ya moja kwa moja wameona umuhimu wa kushirikiana na wasanii wa bongo fleva na bongo movie kuhamasisha uchangiaji huo kwa pamoja ilikuweza kuwashirikisha na wengine.


“TSN, Tanzania sisi Nyumbani, tunaunganisha nguvu ya wasanii hawa kutoka katika tasnia hizi mbili tofauti  kwa lengo la kuhamashisha uchangiaji wa pamoja,”

Alisema mechi hiyo inatazamiwa kuchezwa saa tisa mchana katika uwanja huo wa Taif

No comments: