Thursday, November 3, 2016

Kama unasoma Mkoa wa Dar es salaam masomo ya sayansi,Hii hapa Ahadi Mpya kutoka kwa Mkuu wa mkoa Paul Makonda leo


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh Paul Makonda akipokea msaada wa Madawati yenye Thamani ya Shilingi za kitanzania Million 20 madawati ambayo yametolewa na Uongozi wa Shule ya Kimataifa ya AL MUNTAZIR SCHOOL,Pembeni ni Viongozi wa Shule hiyo wakiongozwa na mwenyekiti wa Bodi Azim Dewji 
 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda leo ameahidi Neema kubwa kwa walimu na wanafunzi watakaofanya vizuri katika masomo ya sayansi katika mkoa wa Dar es salaam akianza na matokeo ya mtihani wa kidato cha nne unaofanyika mwaka huu.

Makonda amesema kuwa Mwanafunzi wa kidato cha nne katika mkoa wa Dar es salaam atakayeongoza katika masomo ya sayansi atapata nafasi ya kusoma Bure kidato cha Tano na cha Sita kwa kulipiwa kila kitu na ofisi ya mkuu huyo wa mkoa na baada ya kumaliza kidato cha sita Atakayeongoza atapewa Shiling Million Mbili kwa ajili ya kuanzia maisha yake ya chuo kikuu jambo ambalo Makonda amesema kuwa analifanya ili kuinua hari ya wanafuzi wa Dar es salaam kupenda masomo ya sayansi.


Aidha katika upande wa walimu Makonda amesema kuwa mwalimu wa masomo ya sayansi ambaye atasaidia shule yake kupata mwanafunzi aliyeongoza katika masomo ya sayansi mwalimu huyo atapata Shilingi millioni mbili kama zawadi kutoka katika ofisi yake na pia mwalimu huyo atapewa nafasi ya kuchagua mbuga nzuri yoyote nchini atakayokwenda yeye na mwenza wake  kwa ajili ya kupumzika na kupunga upepo kwa Siku mbili.
Baadhi ya madwati yaliyotolewa na shule hiyo kama msaada kwa shule za mkoa wa Dar es salaam
Mh Makonda amesema kuwa kutokana na uhaba mkubwa wa walimu wa sayansi na wataalamu wengine na ukizingatia kuwa Tanzania inajiandaa kuwa nchi ya viwanda sasa ameanza Juhudi binafsi kwa ajili ya kuongeza wataalamu wa masomo wa sayansi ili wawe hazina ya Taifa Baadae.

Ahadi hizo Amezitoa leo Jijini Dar es salaam wakati akipokea Msaada wa madawati zaidi ya Mia mbili yenye Thamani ya Million 20 yaliyotolewa na uongozi wa Shule ya kimataifa ya AL MUNTAZIR SCHOOL ikiwa ni msaada wa kuunga mkono Juhudi za serikali karika kutatua tatizo la uhaba wa Madawati Katika Jiji hilo.


Mkuu huyo wa mkoa ameipongeza Shule hiyo kwa Msaada huo ambao utasaidia kupunguza uhaba wa madawati huku akiwataka wadau wengine kuendelea kuunga mkono Juhudi hizo kwa maendeleo ya Elimu ya mkoa wa Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla.






No comments: